Vifo Vya Wanandoa Siku Ya Christmas, Inasikitisha Sana - EDUSPORTSTZ

Latest

Vifo Vya Wanandoa Siku Ya Christmas, Inasikitisha Sana

 


Steven Yamba(44) mfanyabiashara wa nchini Zambia ameripotiwa kumshushia kipigo kikali mke wake wa ndoa Kangwa Mwango(33) na kufariki asubuhi saa tatu Desemba 25 siku ya christmas. Mwanaume huyo alijaribu kumpeleka mkewe  hosptali lakini alipogundua mkewe kafariki na yeye aliamua kukimbilia dukani kununua dawa ya kuulia wadudu akanywa na yeye kufariki dunia.

Polisi nchini humo wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na wamesema uchunguzi wa awali umeonesha mfanyabiashara huyo usiku wa saa moja katika mkesha christmas ndio alianza kumpiga mkewe hadi asubuhi na mke huyo alipoanza kuwa hoi ndio akajifanya kutaka kumpeleka hospitali ambapo alikua kafariki Dunia.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz