Mwanahabari wa BBC Kate Mitchell Apatikana Akiwa Amefariki Dunia Hotelini Nairobi - EDUSPORTSTZ

Latest

Mwanahabari wa BBC Kate Mitchell Apatikana Akiwa Amefariki Dunia Hotelini Nairobi




Mwanahabari wa BBC Kate Mitchell apatikana akiwa amefariki dunia hotelini Nairobi

Afisa mkuu wa polisi Augustine Ntumbi amethibitisha kwamba mwili wa Mitchell ulipatikana katika chumba cha hoteli moja jijini Nairobi siku ya Ijumaa, Novemba 19.

Shirika la BBC pia lilitangaza kifo cha Mitchell ambaye hadi dakika ya mwisho alikuwa akifanyia kazi yake nchini Ethiopia.

" Nasikitika kutangaza kifo cha mmoja wetu Kate Mitchell. Alifariki dunia akiwa jijini Nairobi kwenye chumba cha hoteli," Sehemu ya tangazo hilo kama ilivyonukuliwa.


 
Shirika hilo lilisema bado halijabaini chanzo cha kifo cha Mitchell na kufutilia mbali madai kwamba huenda kilitokana na majukumu yake kama mwanahabari wa kimataifa.



" Chanzo cha kifo cha Kate hakijabaini lakini tunashirikiana na ubalozi wa Uingereza na polisi jijini Nairobi kufanya uchunguzi. Tutapeana usaidizi kadri ya uwezo wetu kwa wapepelezi na kile tunachokijua, hakuna ishara kwamba kifo chake kilitokana na majukumu yake kama mfanyakazi wa BBC," Taarifa zaidi ilisoma.


Kabla ya kuhamishwa na kupelekwa Ethiopia, Mitchell aliwahi kufanya kazi nchini Sudan Kusini na Zambia.






Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz