Mwijaku Afunguka "Nipo Tayari Kutembea Uchi ila Sheria za Nchi Haziruhusu" - EDUSPORTSTZ

Latest

Mwijaku Afunguka "Nipo Tayari Kutembea Uchi ila Sheria za Nchi Haziruhusu"


Muhamasishaji mpya wa klabu ya Simba @mwijaku_1 amegoma kufanya kile alichoahidi hivi karibuni mbele ya waandishi wa habari, kauli yake ya kwamba angetembea utupu bila nguo, endapo klabu yake ya simba ingepoteza katika mchezo wa marudiano wa klabu bingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana.

@mwijaku_1 ambaye pia ni mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm, akizungumza leo kwenye kipindi hicho amedai kwamba alikua tayari kutekeleleza ahadi yake lakini amejua kwamba sheria ya nchi haimruhusu kufanya hivyo.

Ikumbukwe klabu ya Simba imeondoshwa katika Ligi ya Mabingwa Afrika kwa msimu huu na Jwaneng Galaxy ya Botswana baada ya kuruhusu kufungwa bao 3-1 nyumbani kwenye mchezo wa jana jumapili katika dimba la Benjamin Mkapa.


Majina ya Waliochaguliwa Kujiunga na Jeshi la Polisi, Names of Individuals Chosen to Join Tanzania Police Force

Hayo yanajiri baada ya Simba kuruhusu kufungwa mabao matatu nyumbani na kufanya uwiano wa mabao kuwa 3-3 baada ya kushinda 2-0 ugenini hivyo wameondolewa kwa kanuni ya bao la ugenini.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz