Mimi Mars Achafukwa na Wasanii wa Nje Wanapokuwa Nchini na Kupewa Treatment Nzuri Huku Wabongo Wakionekana Takataka - EDUSPORTSTZ

Latest

Mimi Mars Achafukwa na Wasanii wa Nje Wanapokuwa Nchini na Kupewa Treatment Nzuri Huku Wabongo Wakionekana Takataka





MSANII wa kike kunako Bongo Flevani, Mimi Mars ameyatoa yake ya moyoni kwa wadau wa muziki nchini Tanzania ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa hawawaheshimu wasanii wa ndani ya nchi, badala yake wanawaheshimu na kuwashobokea wale wanaotoka nje ya Bongo.


Kupitia Insta Story yake, Mimi Mars ameandika; “Kwa yeyote itakayemhusu; inabidi muanze kuwapa heshima inayostahili wasanii wenu wa nyumbani zaidi hata ya wasanii mnaowaleta kutoka nchi za nje. Ifike mahali wasanii tupaze sauti…”


Hata hivyo, Mimi Mars hajaweka wazi zaidi ni kitu gani ambacho kimemsababisha aseme hivyo, lakini wadukuzi wamesema ujumbe umewafikia wahusika.

STORI; IJUMAA WIKIENDA, DAR




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz