Mauasama "Niliajiriwa Mahali Ndio Maana Nikawa Kimya Kwa Muda Mrefu" - EDUSPORTSTZ

Latest

Mauasama "Niliajiriwa Mahali Ndio Maana Nikawa Kimya Kwa Muda Mrefu"


"Kiukweli mambo ni mengi yalitokea, hapa katikati kuna matatizo nilipata lakini pia majukumu yalikuwa mengi. Mbali na kwamba mimi ni msanii lakini pia nimesomea 'marketing' unapokuwa unapata fursa mbalimbali ambazo zinalipa kwa wakati huo inakuwa sio mbaya kuzifanya"

"Hiyo taasisi ambayo nilikuwa nafanya kazi ilikuwa na Mawasiliano mazuri na Management yangu walinishawishi tukafanya kazi pamoja baadae nikaona nifanye muziki kitu pekee ninachokipenda na pia nimewekeza huko kwa miaka mingi. Na pia sikutaka kuwapoteza mashabiki wangu na kelele za unarudi lini, natoa Ngoma mpya lini zilikuwa nyingi zikanifanya nirudi rasmi kwenye muziki"

"Lakini pia nilipatwa na matatizo na wakati nilipokuwa nikiyakabili yale matatizo nilikuwa natamani kutoa nyimbo na kurudi kwenye muziki. Ikabidi nitoe wimbo. Kwa sasa hivi nimepumzika kufanya kazi na hiyo taasisi ila tupo vizuri na nimerudi rasmi kwenye muziki"

"Nilishindwa kufanya muziki kwa kipindi chote kwa sababu ya kazi. Kwa sababu nilikuwa kazini muda wote na pia nimesomea mambo ya masoko" @mauasama,





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz