Adam Mchomvu Afunguka "Wasafi Wakinitaka Wajipange Vizuri" - EDUSPORTSTZ

Latest

Adam Mchomvu Afunguka "Wasafi Wakinitaka Wajipange Vizuri"

 


Mtangazaji mkongwe tokea CLOUDS MEDIA GROUP (Clouds Fm), @adamchomvu akiwa kwenye kipindi cha Big Sunday Live cha Wasafi Tv amejibu swali la shabiki aliyeuliza ikiwa Wasafi watamuhitaji,je ataihama Clouds?

Amedai inabidi wajipange sana maana hana mpango wa kuhama Clouds,alipokuwa anatamani kuwa Presenter alichagua media iliyokaa kijanja na akaichagua Clouds, akidai pia imemkuza kwahiyo atabaki kuwa hapo kuwainspire wengine.

Kingine Mchomvu amedai anachokifanya @diamondplatnumz

Anajiwakilisha yeye lakini pia ni sifa kwa taifa zima,hivyo anapaswa kusapotiwa na wote,kilichotokea kabla ni mikakati ya kibiashara.

200 Job Opportunities at PCCB / TAKUKURU, Investigation Officers

Kwenye kutoa marks za Lyrics amempa Dullah Planet 4 kisa tu kujiita rais na kudai ameibeba Bongo Flava mabegani,kitu ambacho amepinga akisema amepambania huu muziki na hajawahi jiita rais,hata Diamond anajua namna alivyompambania kipindi anatoka hadi leo tunamuona Diamond huyu.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz