Jack Wolper Achachamaa Kuwashtaki Wanaomsema Mtoto Wake Mitandaoni - EDUSPORTSTZ

Latest

Jack Wolper Achachamaa Kuwashtaki Wanaomsema Mtoto Wake Mitandaoni




MUIGIZAJI maarufu wa Bongo Movie Jackline Wolper amevunja ukimya kwa kueleza kwamba mtu yoyote ambaye atamchafua,kumdhalilisha au kumkashifu mtoto wake Pascal a.k a P atamchukulia hatua za kisheria.

Wolper mwenye weupe na uzuri wake ulioambana na umbo lenye kuvutia ,amevunja ukimya huo leo Septemba 16, 2021 ambapo ameweka wazi hawezi kumjibu kila mtu mtandaoni ,hivyo sheria itachukua mkondo wake.

"Siwezi kumjibu kila mtu atakayekuwa akimdhihaki mtoto wangu bali nitatumia sheria zaidi na kwa sasa watu wawili wa mitandaoni kurasa za udaku nimewafikisha katika sheria ndio sababu ya kutoona picha zangu za ujauzito hazisambazwi zikiwa na matangazo ya kuhusu tiba za afya,"amesema.

Akipiga stori zaidi Wolper ametumia nafasi hiyo kueleza sababu za kutomuonyesha kwa muda mrefu katika Mitandao ya kijamii kama ilivozoeleka kwa mastaa pamoja na watu mbalimbali mara baada ya kujifungua.

Wolper ambaye amepewa ubalozi katika duka la nguo Sweetrolah amesema hivi ;"Niliingia mkataba na Kampuni ya Sweetrolah tangu nilivyokua na ujauzito wa miezi tisa, nikaona niwe wa kipekee kabisa nisisambaze picha za mtoto mahali popote pale."

Amefafanua kuwa ubalozi wa P atautumia kama nafasi pekee ya kutangaza nguo na vitu mbalimbali vitakavyokua vinapatikana dukani hapo."Wakati tunasaini mkataba wa ubalozi niliomba vitu vitatu ikiwemo mashabiki zangu kupata vitu katika duka hilo ambavyo vitakua rahisi kumudu kununua, hivyo nashukuru kwa kufanikishiwa hilo."




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz