Gari la Marehemu Tupac Shakur lauzwa bilioni 4 - EDUSPORTSTZ

Latest

Gari la Marehemu Tupac Shakur lauzwa bilioni 4






Gari la Marehemu Tupac Shakur ambalo alikuwa akilitumia yapata miaka 25 iliyopita aina ya BMW 750IL la mwaka 1996 linauzwa kwa dola milioni 1.7 za Marekani ambazo ni takribani Bilioni 4 za Kitanzania.

Gari hilo ambalo alipigwa nayo risasi akiwa ndani yake usiku wa Septemba 7, mwaka 1996 na kupelekea kufariki dunia siku sita baadaye kufuatia shambulio hilo ambalo liliruhusu risasi nne kuingia mwilini mwake, akiwa na mtayarishaji Suge Knight.

Kwasasa liko kwenye eneo la maonyesho ya magari ya watu maarufu huko Las Vegas limekarabatiwa, mashimo yaliyotokana na risasi yamezibwa na kurudishwa katika hali yake mpya.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz