Watoto wachanga watekwa nyara hospitalini Nigeria - EDUSPORTSTZ

Latest

Watoto wachanga watekwa nyara hospitalini Nigeria

 


Watu wenye silaha wamewateka nyara watoto wachanga, wauguzi na walinzi wa usalama katika hospitali iliyopo kaskazini magharibi mwa Nigeria, polisi imesema.

Majambazi wa eneo hilo walifanya mashambulio ya mfulurizo kwenye kituo cha polisi na kituo cha taifa cha kifua kikuu na ukoma, kabla ya kutorokea msituni.

Afisa wa serikali katika eneo hilo amesema jeshi limeanza juhudi za kuwatafuta waathiriwa.

Takriban watu saba waliuawa katika shambulio kama hilo lililotekelezwa na watu wenye silaha mwishoni mwa juma katika jimbo la Kaduna.

Utekaji nyara kwa ajili ya kikombozi ni wa mara kwa mara nchini Nigeria.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz