"Nisamehe Metacha kwa kukutabiria mabaya, Waliokutukana jana kuna siku watakushangilia kama shujaa" Haji Manara - EDUSPORTSTZ

Latest

"Nisamehe Metacha kwa kukutabiria mabaya, Waliokutukana jana kuna siku watakushangilia kama shujaa" Haji Manara





Afisa habari wa timu ya Simba amemuomba msamaha golikipa wa Yanga Metacha mnacha kwa like alichodai kumtabiria Jambo baya na ndani ya muda mfupi kutokea Kama alivyosema.
Manara alitoa mfano wa Melinda mlango wa nje ambaye alileta mzaa golini na kusababisha kujifunga kizembe.

Manara kwenye post ya kwanza alisema "Pata picha kosa hili ndio alifanye Metacha tarehe tatu,,,Wallah Utopolo wanamla nyama mchana kweupeeeee , Na ngozi anaondoka nayo Mzee Mpili kuipeleka Ikwiriri "

Lakini kwenye mchezo wa Jana Metacha alifanya kosa lililompelekea kupata lawama nyingi adi kusimamishwa.

Kupitia ukurasa wake wa instagramu manara ameandika; Mdomo unaumba..

Juzi niliweka video inayomuonyesha kipa mmoja huko Ulaya akifanya kosa lilioigharimu timu yake na kuandika ikitokea kosa kama lile akfanya kipa Metacha,,basi Utopolo watammeza!!

Jana Kwa bahati mbaya sana kama ilivyo Kwa Binadaam wote ada yetu ya kukosa, Metacha akakosea,,kilichotokea sitaki kukiongelea tena.

Ila nilitaka kumwambia Sorry tu Kwa kipa huyu bora kabisa ,,,tambua hzo ndio changamoto za maisha ya mcheza soka,,Waliokutukana jana kuna siku watakushangilia kama walivyowahi kukuona shujaa wao huko nyuma,,,,,Muhimu uwe na moyo mgumu zaid na usilipe tena matusi,,,,ile ishara sio stahiki ya wanazi wasiojua kitu kuhusu football,,,,wao kwao Simba na Yanga hazipaswi kukosea na Wachezaji wake ni Malaika always!!

Na nisamehe kwa post yangu ya juzi iliyokutabiria yaliyotokea jana,,ww ni Star na utaendelea kuwa Star Insha'Allah






Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz