MANGE KIMAMBI amshauri HARMONIZE ‘Mashabiki wako karibia wote ni wa ALIKIBA, usishindane naye’ - EDUSPORTSTZ

Latest

MANGE KIMAMBI amshauri HARMONIZE ‘Mashabiki wako karibia wote ni wa ALIKIBA, usishindane naye’


MANGE KIMAMBI amshauri HARMONIZE ‘Mashabiki wako karibia wote ni wa ALIKIBA, usishindane naye’
Mange Kimambi Amenadika haya:

 
Mdogo angu upande wa mama huyu….

Fans wako karibia wote ni fans wa Kiba sasa jaribu usiwe unashindana nae unakuwa una kosa support. Kama mi dadako Kiba angekuwa hayuko hewani sasa hivi ningesimana na wewe tuwashinde wale 🤣🤣🤣 ila sasa ona hata nyimbo yako nimeposti ili nikupe hii meseji. Yani the only way na wewe ungeshine kipimdi hiki ilibidi fans wa Kiba wamwache Kiba waje kwako kitu ambacho ni kigumu.

Inabidi uwe very strategic kwenye ku-release kazi zako. Hapa marekani wasaniii hawaachii kazi hovyo wanatumia akili kubwa mnoooooo katika kuachia ngoma. Timing ya kuachia kazi is almost as important as uzuri wa nyimbo. Kwa mfano Rihanna aachie ngoma kali hutokaaa usikue after 2 days Beyonce nae anaachia ngoma. The problem ni kwamba wote wanataka Ngoma zao ziwe#1 kwenye billboard charts sasa mkiachia wote same time lazma mmoja awe 2. Na wasanii wakubwa kutokuwa #1 ni big deal mnoo. So inabidi uachie kazi muda ambao hakuna hit kubwaaaa ili uwe namba 1. Hata kama only for 1 week ila angalau uiguse number 1.

Ona hata Jide kaachia ngoma kali ila watu kama hatujaiona sababu tupo busy na watu wawili. Jide angetulia akaachia ngoma baada ya wiki 3 hivi ange hit kinoma noma. Ila muda hakuuchagua vizuri. Timing is crucial.

Alafu huku wasaniii wanatangaza hadharani tarehe gani ataachia ngoma. Kwahiyo kila mtu anakuwa anasubiria. Drake hawezi kutangaza anaachia ngoma tarehe flani alafu Chris Brown akamvizia ile kaachia tu na yeye kesho akaachia. Mmoja wao ana risk kuwa namba 2 kwenye billboard charts. Mara chache mnoooooooo msaniii mkubwa anaachia ngoma by surprise. Na hata akichia kwa surprise ana hakikisha hakuna ngoma iliyoshika attention za watu.

Kuna kazi ngumu sana inabidi ifanyike ya kuua team Dai na Team Kiba hizi team zinauwa wasaniii wengine. Inabidi tusapoti wasanii woteNa hiyo Kazi inabidi ianzie kwetu sisi vigagula. Ila na wasanii nao wapeane muda wakuachia kazi ili wote wapate attention kubwa, wasigawe mashabiki kwa wote kuachia kazi same time.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz