Hatma ya Mdude Kujulikana Leo - EDUSPORTSTZ

Latest

Hatma ya Mdude Kujulikana Leo

 


Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya leo Juni 28, 2021, inatarajiwa kutoa hukumu ya kesi inayomkabili kada wa CHADEMA, Mdude Nyangali. Mdude anakabiliwa na mashtaka ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroin, gramu 23.4.

Juni 14, 2021, Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya iliahirisha kutoa hukumu dhidi ya kesi yake kwa kile kilichoelezwa kuwa hukumu bado haijakamilika pamoja na mambo mengine ambayo yalikuwa nje ya uwezo wa Hakimu.

Mdude anakabiliwa na makosa ya usafirishaji wa dawa za kulevya aina ya Heroin kinyume cha sheria cha udhibiti dawa za kulevya namba 5 ya Mwaka 2015.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz