Ajali ya ndege Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo - EDUSPORTSTZ

Latest

Ajali ya ndege Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

 


Watu watatu wameripotiwa kupoteza maisha baada ya ndege ya kibiashara iliyokuwa imewabeba kuanguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka mkoa wa Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya kitaifa, ndege hiyo ya kibiashara ilianguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka Uwanja wa ndege wa Kavumu.

Wahudumu 2 na abiria 1 walifariki katika ajali hiyo.

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijatambulika.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz