FANYA HIVI ILI UMPATE UNAYETAMANI AWE WAKO - EDUSPORTSTZ

Latest

FANYA HIVI ILI UMPATE UNAYETAMANI AWE WAKO


 NI kweli wapo waliokutana katika daladala na baada ya siku chache wakafunga ndoa na leo wanaishi maisha ya amani na furaha.

JIUNGE NA GROUP LA WAKUBA HAPA 18+ HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA

Wengine walionana ufukweni na ndani ya wiki kadhaa wakaingia katika ndoa inayowafanya wafurahi na kuwa na amani karibu muda wote. Hayo yanawezekana kutokea.

Unaweza kukutana katika siku chache na mwenzako na kisha baada ya muda kidogo, mkaingia katika uhusiano. Inawezekana. Ila ni moja kati ya kumi!

Pakua App ya 'EDUSPOTSTZ (LITE VERSION)' Uweze kufurahia Habari zote za Mapenzi; Udaku, Ajira na Michezo kila siku Ipo Google Playstore, Kwa Ku BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD Kwenye Simu yako Utasoma habari zote hata kama hauna MB

Wengi waliokutana kwa namna hiyo na kuharakisha kuingia katika uhusiano ni wenye kujuta na kulaumu maamuzi yao. Mapenzi ni suala pana sana.

Si suala linalohitaji papara au uamuzi wa jazba. Kuna misingi na kanuni fulani inabidi kufuata ili uweze kufikia katika uhusiano wa amani, raha na thamani.

Ndiyo, mapenzi ni hisia zinazokuja zenyewe bila kulazimishwa wala kushurutishwa na mtu. Ni hisia zisizochagua mahala pakuonekana wala kujionesha.

Si sahihi kusema eti mpenzi wa kweli nitampata chuoni au kazini, hapana. Wengi walikutana huko wakaambulia maumivu na madhila.

Na wengi walikutana huko wakajikuta wanaingia katika ukurasa wa furaha na amani ya maisha yao. Hakuna eneo wala nchi ya kupata mpenzi wa kweli. Si shuleni, hospitali wala baa.

Kila sehemu ina nafasi yake ya kukupa furaha katika maisha yako na karaha kupitia mapenzi. Suala ni umakini na kufuata misingi bora ya uanzishaji wa uhusiano.

Kuna watu nawajua walikutana sehemu za starehe, sehemu ambazo kwa wengi huamini kuwa si salama kwa kukutania na watu wa maana.

Ila baada ya muda fulani wakaingia katika uhusiano na leo ni miaka kadhaa kuna amani na furaha ndani ya ndoa zao.

Kuna mwanamuziki anaitwa Benjamini alikutana na mpenzi wake katika maandalizi ya video ya wimbo wake.

Alisema alikuwa akitafuta wanawake kwa ajili ya kucheza ndani ya ile video. Alitafuta wasichana wengi ila mmoja wapo alikuwa huyu ambaye leo anamwita mke.

Japo msichana yule hakuwa tayari kwa ajili ya video ile ila baada ya hapo waliwasiliana na matokeo yake imezaliwa ndoa ya furaha na amani kwa mujibu wa maelezo yake.

Suala ninalotaka ulielewe hapa ni kuwa hisia hazina mahala wala muda wa kuonekana. Suala ni umakini na kushusha hali ya haraka katika uanzishaji wa uhusiano wako.

Ndiyo, umekutana na mtu unayeamini unampenda katika daladala ila je, unafuata hatua gani kuingia naye ndani ya uhusiano?

Wengi watachukua namba ya simu leo saa sita mchana, kesho kutwa saa kumi jioni atatongoza. Hapa ndipo wengi tunapoumia na kila siku kulia katika uhusiano.

Anzisha naye urafiki wa karibu usiohusisha mambo ya mapenzi. Tena kuwa mjanja wa kutoonesha kwa pupa hisia zako juu yake ili upate muda wa kumsoma kwa umakini na kumjua jinsi alivyo.

Usiwe na papara, unaweza kuwa naye katika hali hii hata kwa zaidi ya miezi mitatu au minne. Suala si mapenzi ya kweli?

Sasa haraka ya nini? Vijana wengi huwa na pupa ya ngono na matokeo yake wanawahi kutaka kuanzisha uhusiano haraka na kujikuta wakiingia katika majuto na maumivu yasiyokuwa na mfano.

Kuwa makini na kauli na matendo yako katika hali hii. Jitahidi kuwa na ule urafiki utakaokufanya umjue yeye vizuri, marafiki pamoja na nasaba yake.

Hili litakusaidia kumjua vizuri zaidi na kujua yeye hasa ni mtu wa aina gani.

Tunapozungumza kuwa inabidi ujuane na mtu unayetaka kuanzisha naye uhusiano, haina maana ujue jina lake tu  na upate namba yake ya simu. Hapana! Inabidi umjue hasa yeye nani ana mipango gani na mtu wa aina gani.

Ujue tabia yake halisi na hili linawezekana tu kama utamfanya awe rafiki yake huku ile dhamira yako ya kutaka kuanzisha naye uhusiano ukiificha katika hali fulani ili asiweze kuijua na matokeo yake akawa anaonesha tabia za kuigiza.

Pata GB 10 Mtinadao yote BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


JIUNGE NA GROUP LA WAKUBA HAPA 18+ HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz