Mwili wako ni wa Thamani sana. Mwili wako ndio utu wako. - EDUSPORTSTZ

Latest

Mwili wako ni wa Thamani sana. Mwili wako ndio utu wako.


Ebu Tunza Mwili wako nao Ukutunze. Uheshimu Mwili wako nao Utakuheshimisha.
Si kila mtu wa kuushika Mwili wako. Usitumie Mwili wako kama kitega uchumi, Usitumie Mwili wako kama dhamana ya kupata vile unavyohitaji.
Usitumie Mwili wako kama Njia ya kupata Mume Atakayekuoa. Kama Mungu amepanga Uolewe utaolewa tu
dada yangu hata bila ya kufunua Sketi yako. Muamini Mungu Yeye ndiye aliyeshikilia maisha yako.
DADA ZANGU NI VIZURI KAMA MKIYAFAHAMU HAYA..!
Mwili wako sio Maonesho, kila mwanaume auone.
Mwili wako sio Mdoli kila mwanaume Auchezee.
Mwili wako sio dampo, upokee kila uchafu wa mwanaume.
Mwili wako sio Mali ya umma kila mwanaume akutumie.
Mwili wako sio kiburudisho, kila mwanaume Ajiridhishe.
Mwili wako sio pazia la Sebuleni, kila mwanaume Akufunue.
Mwili wako sio karanga za kutembezwa mtaani kila mwanaume
Akuonje Utamu wako.
*********************************************
*********
Kuna mtu mmoja tu anayestahili kuugusa Mwili wako, kuuona Mwili wako, kuujua Uzuri wako.. Msubiri, Usiwe na Haraka, Mungu atamleta kwako. Endelea Kusubiri.
JITUNZE, JITHAMINI, JIKUBALI NA JIAMINI..!




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz