Haya ndio maneno mwanamke hutumia akiwa anachepuka. - EDUSPORTSTZ

Latest

Haya ndio maneno mwanamke hutumia akiwa anachepuka.

NDOA NA MAHUSIANO: June 2015


Wapenzi huwa wanasalitiana kwa sababu mbalimbali na kusalitiana huko sio kuwa hawafurahii uhusiano waliokuwa nao.
Ingawa wanaume wanaonekana kuongoza zaidi kuchepuka kwenye mahusiano lakini hata wanawake pia husaliti ila wao huwa makini na wajanja sana na ni vigumu  kuwanasa.
Watupipo inakuletea maneno ya uongo yanayotumika mara nyingi na mwanamke anapokuwa anacheate.
Ni kama kaka yangu.
Kama mpenzi wako akiwa anatumia muda mwingi na mwanaume mwingine au kuchatt unapaswa kuwa makini.Inakua mbaya zaidi kama pale utapomuuliza na kujibiwa “Huyu ni rafiki yangu ni kama kaka kwangu sio vinginevyo’ hii lazima ikupe uoga kuna uwezekano mpenzi wako akawa anakusaliti na kaka yake huyo.
Nilikuwa na mashosti wangu.
Kama unampigia mwanamke wako simu na anakuwa hapatikani kwa muda mrefu na akipatikana badae husema kuwa alikuwa kwa rafiki zake wa kike hakutegemea kama angechelewa fanya utafiti zaidi.Wanawake mara nyingi hutumia mgongo wa marafiki zao wakiwa wanampango wa kucheatte.Wanawake hao huwa wanateteana siku zote kwa hiyo usiwaamini sana na wao.
Nachelewa kutoka kazini.
Hii ndio hutumika sana.Utaambiwa usinisumbue kwenye simu niko busy na pia ntachelewa kurudi nyumbani.Hii inamaanisha kuwa huenda akawa na mwanamume mwingine na usumbufu wako ni kitu hakitaki kwa muda huo.
Kuwa na wewe ni kitu kikubwa sana kilichotokea kwangu.
Kama mwanamke wako ghafla tu kaanza kukwambia maneno ya kukuona wa thamani sana ni pengine ni baada ya kujiona mkosaji na kujaribu kufanya kitu kurekebisha hisia zake.Utaambiwa maneno mengi kama ingekuaje kama asingekuwa na wewe mara we ni lulu kwake stuka chukua muda tathimini thamani hiyo imetoka wapi ghafla.
Nahitaji muda kidogo.
Mwanamke anapenda kuwa na ukaribu na mwanaume ambaye anampenda kweli.Ni kawaida na kiafya safi kwa mwanamke alioko katika mahusiano kupunzika na kuwa na muda wake.Lakini ni dalili ya hatari pale mwanamke huyo unapoona hana tena muda na wewe kwa kigezo cha kumwacha kidogo hapo kunadalili nyingine ya kuwa na mtu anaependa kuwa nae sio wewe tena.
Sikusaliti mpenzi.

Nafikiri hata hii ni common sana kwa mwanamke anae cheatte.Ni nature kwa binadamu kukana vitu ambavyo mara nyingi wanakuwa wakivifanya.Hasa pale anapokuwa anakwambia hakusaliti  huku hata hukumuuliza stuka! unasalitiwa wewe angalia kwa undani zaidi utagundua.
Usisahau kushare post hii.👍 Share facebook, twitter, Google+ n.k bila kusahau WhatsApp! Share kote wenzio nao wasome

Most Recent





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz