TOFAUTI KUBWA KATI YA MWANUME NA MWANAMKE - EDUSPORTSTZ

Latest

TOFAUTI KUBWA KATI YA MWANUME NA MWANAMKE

Image may contain: 1 person, child, wedding, outdoor and water

Kila Mwanaume ametokana na Mwanamke vivyo hivyo kila Mwanamke ametokana na Mwanaume!
Lakini tofauti kubwa iliyopo kati ya Mwanaume na Mwanamke kuijuwa THAMANI ya mwenzie ni kubwa sana, Mwanamke anaijuwa THAMANI ya Mwanaume kwa sababu yeye ni MAMA... Na ki biolojia Mama hana mbadala kwa nafasi yake, Mwanaume huijua THAMANI ya Mwanamke kwa mahitaji yake Kwani yeye huamini Mwanamke hana nafasi nyingine ila sehemu ya BURUDANI YAKE😭
Mgongano huo wa ki mtazamo ndo umepelekea WENGI KUINGIZANA KWENYE MAUMIVU JUU YA MAPENZI! Wanaume wangemtazama Mwanamke kama ambavyo MUNGU alimuumba Mwanamke kwa heshima kubwa, Mwanamke ni MAMA na pia ni TULIZO LA MOYO WA MWANAUME🤦🏾‍♂
lakini wanaume wengi huishi na Mwanamke kwa mtazamo mmoja kwamba MWANAMKE NI MSAIDIZI WAKE... Mungu alipomwambia ADAM nimekupa Mwana Mke ili awe msaidizi wako haikuwa na maana kama ambavyo wanaume tunaichukulia, Maana ya MUNGU ilikuwa Mwanamke kumpa tulizo Mwanaume😋
Sasa hivi ili Mwanamke aweze walau kumpata Mwanaume ambaye anadhani wanaendana ANAWAJIBIKA KUGHARAMIA PENZI kisa tu Mwanamke amekuwa mdhaifu kwa Mwanaume huyo, Wanaume mmekuwaje
Heshima ya Mwanaume kuwajibika kwa Mwanamke wake, Lakini hii tabia mnayo hiyo ndo imepelekea wanawake kutudharau Kwani NI MWANAMKE GANI ATAKUHESHIMU NA ANAKUHUDUMIA
Mwanamke hakuumbwa kutoa kitu ila UPENDO sasa wewe ukitaka akupe vyote Yaani unataka akupende na akulee wallah TARAJIA KUWA MHANGA WA PENZI😂
Hawakuumbwa hivyo tunawalazimisha tu hata kununua nyama nyumbani, Mwanamke hujisikia fahari sana aonapo ana mwanaume anasimamia majukumu yake💃
Wanaume wote wangejua umuhimu wa MWANAMKE kama ambavyo wanajua umuhimu wa MAMA nadhani kesi nyingi zingekuwa MWANAUME ANA WIVU HUYUUUU😂
Tofauti na sasa kesi nyingi ni MWANAUME MHUNI HUYU🙆🏿‍♂
Wallah kama MUNGU asingekuwa na huruma ungekuta Wanaume wanaotesa wake zao WANARUDISHWA MATUMBONI MWA MAMA ZAO ili waondoke kwenye sura ya DUNIA😂
Ukimpenda Mwanamke ATAKUPENDA💘
Ukimheshimu Mwanamke ATAKUHESHIMU🙏
Kinyume cha hayo nae ana moyo ujue, PANIC AT YOUR OWN RISK
#Elista_kasema_ila_Sio_Sheria 




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz