SIO KILA ANAYEONYESHA KUKUPENDA ANAKUPENDA KWELI ,VINGINE NI MTEGO. - EDUSPORTSTZ

Latest

SIO KILA ANAYEONYESHA KUKUPENDA ANAKUPENDA KWELI ,VINGINE NI MTEGO.


Huyu Mwanaume anasema ilikuwa siku ya birthday yake hivyo mke wake akonyesha kusahau kuwa ni birthday ya mme wake hivyo hata hakumuwish happy birthday, mme akajisikia vibaya kweeli,kuna ile hata kabla haijawa asubuhi watu wanaviziaga saa sita kamili anakuimbia happy birthday au anakutumia msg ,lakini kwa huyu Baba ilikuwa tofauti mke hakumuwish usiku ule,asubuhi kulikpokucha akaamka na kujua hapa mke wangu lazima ataniambia happy birthday na suprise juu na asubuhi nayo kimya.

Kilichomuuma huyu baba ni kwamba hadi watoto wake wakamsahau,wazazi wake hasa Mama nao ikawa kimya.
Na hata wafanyakazi wenzake hakuna aliyeonyesha kukumbuka siku hiyo ya muhimu kwake(Birthday)
Roho ikamuuma akajisikia kama kutopendwa.Mawazo yakamjaa akahisi kulia na dunia akaiona chungu.
Akiwa njiani kuelekea ofisini akawa anaaangalia simu yake labda hata kuna aliyemkumbuka hakuna.Mmh mme akasema wacha niende kazini isiwe shida labda saa nne muda wa chai yumkini akaja kunifanyia suprise ofisini mmh saa nne nayo kimya hakuna cha simu wala msg ya happy birthday. Facebook kimya,whatsup status kimya.
Alivyofika kazini akaingia moja kwa moja ofisini kwake.Ile anaingia mara secretary wake akamkimbilia na kumwambia HAPPY BIRTHDAY BOSS.
Waoo moyo wa boss ukafanya paaa,akajiona so special yaani.
Secretary hakuishia hapo akamuomba mchana amtoe lunch kama hutojali.Boss anaanzaje kukutaa kwa mfano?huku mke na wengine hawajaona thamani yake.
Mchana wakaenda lunch,secretary akamuomba waende wote kwake
Boss akaona eeh waa,ngoja niende nikamkomeshe huyu mke anayeonekana kutonijali na kusahau siku yangu ya muhimu.
Haoo mpaka kwa bidada,mwanaume yuko tayari kwa lolote maana sio kwa upendo huo wa birthday alioonyeshwa.
Mwanaume akatoa nguo zake zote yuko tayari kutoa asante kwa good treatment, mara dada anasema wacha niende chumbani mara moja nakuja.
Akamwambia sawa huku mwanaume akiona kama anacheleweshwa.
Mara dada anatoka chumbani na Team.Team ikiwa na mke mtu,watoto wake,wazazi wake na wafanyakazi wenzake huku wamebeba cake wote kwa pamoja wakasema SUPRISEEEEE huku mme yuko kwenye kochi Uchi.
Ungekuwa wewe ungefanyaje??
FUNZO
Jifunze kujipenda kwanza wewe!usisubiri wengine.
Sio kila anayekuonyesha upendo anakupenda kweli kutoka moyoni vingine ni mtegoooo.
Hahahah HAPPINES IS A CHOICE
Winnie Kilemo




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz