OGOPA SANA! SANA! SANA! MWANAUME ANAYEKUJA KWAKO KWA GIA HII! - EDUSPORTSTZ

Latest

OGOPA SANA! SANA! SANA! MWANAUME ANAYEKUJA KWAKO KWA GIA HII!

Image result for UNAINGIA KWENYE MAHUSIANO; ACHA KUMLINGANISHA WA SASA NA WAZAMANI!
Anakutongoza, unajua kabisa ni mume wa mtu na unamuuliza wewe si umeoa? Anakaumbia ndiyo lakini anaanza kukuorodheshea matatizo lukuki ya mke wake, mwisho anamalizia kwa kukuambia kua isingekua ni watoto tungekua tushaachana. Baada ya hapo anajifanya kukupenda, anakujali kuliko mke wake, anakushirikisha katika mambo yake ya maendeleo na kama alikua anajenga anakupeleka mpaka site. Yeye sasa anakuhudumia vitu vidogo vidogo, kama vocha, chakula, vinywaji na vitu vingine ambavyo hata mbuzi anaweza kujihudumia navyo!
Lakini kila siku anonyesha dalili za kumuacha mke wake, yaani mpaka wakati mwingine unajihidi ndoa na kuona kama vile kashamuacha kwani yuko comfortable sana na wewe na wakati mwingine hata baadhi ya marafiki zake na ndugu zake wanakujua. Lakini hamuachi sanasana anakuambia anaangalia namna ambavyo ataachana naye ili isiwaathiri watoto! Whoooooh! Wanaume tunajua kudanganya na dada zangu mnajua kudanganyika, anakuruhusu mpaka umpost, sasa kwakua anakushirikisha katika mambo ya maendeleo unajiona mke kabisa na wakati mwingine hata unakua na kakiburi ka kumpigia mkewe na kumtukana.
Sasa hapo unajikuta unachangia mambo yake ya maendeleo, anajenga anakuambia nina shida flani unatoa, ana matatizo kazini unamsaidia kuyatatua, anataka kununua gari unamuongeze ananunua au hata wewe una gari anakua analitumia kama lake. Mnavuka hatua anakuambia mfanye biashara pamoja, labda wewe ulikua na biashara unaanza kumshirikisha! Doooooh! Hawa watu wanajua kushauri aisee, yaani dakika mbili una tatizo la kibiashara kashakuunganisha na mtu au kakuambia namna ya kulitatua na matatizo yako anayachukulia kama yake, lakini bado anakuambia “Nataka kumuacha mke wangu taratibu!”
Naaandika huku nacheka na kusikitika kwakua nina uhakika kwa asilimia mia kuna mtu atasoma hapa na anafanyiwa hivi hivi lakini atajiambia “Mimi wakwangu ni tofauti! Mke wake ndiyo mwenye matatizo!” tena anaweza kuchukua na mkopo kabisa na kumpa mwanaume wafanye kitu flani cha maendeleo. Nikuambia tu Dada huyo mwanaume ni tapeli na nikuhakikishie kwa asilimia mia moja hauko peke yako anayekufanyia hivi, kila mwanaume ana staili yake ya kutongoza na hii ndiyo staili yake. Hivyo wakati ukijiona spesho, wakati ukijiona labda sijui wewe wa dhahaabu jua kua jua kuna binti mwingine kama wewe ambaye naye anachukua mkopo na kumpa jamaa.
Naomba niwaambie kitu kimoja, hili naomba mpigie mstari kabisa, wanawake wengi wana matatizo lakini hakuna, narudia hakuna, narudia hakuna mwanaume ambaye anaumizwa kweli na kuteswa na mkewe ataenda kutangaza! Hakuna! Kwa mwanaume ni kama kaa aibu flani kusema mke wangua nanifanyia hivi, ananifanyia vile na bado kuendelea kubaki naye, ni aina flani ya ufala na wanaume pamoja na kwamba tunaumia sana lakini tunaficha, ukiona mwanaume anatangaza matatizo ya mkewe basi jua yeye ndiyo kichomi hivyo anatangaza kwa sababu kuu mbili.
Sababu ya kwanza ni ili kumchafua mwanamke, ili yeye kuonekana mwema mbele ya jamaii na mbele yako, na sababu ya pili ni kwakua ndiyo staili yake ya kutongoza. Kila mwanaume ana aina ya mistari yake ambayo huitumia wakati wa kutongoza na hujirudiarudia. Mwanaume wa namna hiyo alikua akitongoza hivyo tangu akiwa shule ya msingi, anakua analaumu mwanamke mmoja ili kupata mwingine. Kwakua wanawake nao hupenda kusifiwa, basi hii ni njia rahisi zaidi ya kumpata mwanamke kwa kumuonyesha kua yeye ni bora kuliko mwanamke mwingine.
NB; Najua huamini hivyo hembu mchukulie huyo mwanaume mkopo au muache boyfriend wako kwaajili yake kwakua uonaona eti yeye anajali sana anajibu SMS kwa wakati. Ukija kuumizwa nitumie kisa chako hapa ili na mimi ukurasa wangu unoge maana si unapendwa bwana subiri atamuacha mkewe taratibu na wewe utaolewa taratibu. Ila usahau ku #SHARE maana kuna Dada huko anatamba kua anapendwa sana kuliko mke wa jamaa! Ashajiona Mama kwenye nyumba kwakua kapelekwa na site kuona ujenzi!




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz