KWANINI WANAUME WANALALAMIKA KWAMBA WANAWAKE WA SASA WANAPENDA HELA?? - EDUSPORTSTZ

Latest

KWANINI WANAUME WANALALAMIKA KWAMBA WANAWAKE WA SASA WANAPENDA HELA??

Young Couple Making Pizza In Kitchen Together Stock Photo - 41146765
Kwanini wanaume wanalalamika wanawake wa sasa wanapenda hela? Ni kwa sababu kizazi hiki cha wanaume ni WACHOYO... kawaida ya MAPENZI ili Mwanaume apewe heshima na mkewe ni wazi anawajibika kutekeleza majukumu yake kama MUME! Kinachowatesa wanaume wa sasa WANAKWEPA MAJUKUMU YAO na kutaka uwiano na wake zao Yaani MKE anunue mboga na MUME anunue unga HUO NI USHENZI kabisaaa😤
Heshima ya MUME kwa mkewe ni kujua mwenza wake anahitaji nini kwa sasa ili amtimizie kwa wakati, Ukiona Mwanaume analalamika sana kuhusu Mwanamke eti anapenda hela ujue ALI-BET HUYO🤣🤣
Nani kakwambia Mwanamke anapenda hela? Acha ushamba huo, Wanawake by nature ni viumbe tegemezi sasa wewe unataka Mwanamke mpaka akuombe? Mwanaume makini anaingia mfukoni anatoa hela bila kuhesabu na kumpatia mkewe, Ni wajibu wako wala sio ombi Man, Hivi unajua heshima ya Mwanamke wewe? Jiangalie unyayo mpaka utosi wako n then mtazame mkeo uone mlivyo tofauti, Kiumbe MWANAMKE ni kiumbe aghari eboooo😳
Wanaume mnalalamika Wanawake wanapenda hela? Ninyi mnapenda nini kwa wanawake🤷🏽‍♂ Mnajua hata sabuni za manjano zinanunuliwaje? Hebu acheni hizo bwana, Mwenzio ananunua mafuta, sabuni, Pands na mengineyo kuitunza hiyo inawapaga kiraruraruuuuu😇 halafu ukiombwa elfu kumi mara mbili unahisi vibaya? Heshima ya MUME kwa MKEWE ni KUHONGA👌
Ukiona nakupotosha kaa kimya ili uje kusaidiwa na wanaume wenZio wanaoijuwa thamani ya Mwanamke 🤰🏼
Wanawake komaeni hivyo hivyo, Mkono mtupu haulambwi, akiona vipi ASEPEEE tu maana hakuna namna, HAPPY INTERNATIONAL WOMEN'S DAY.
#Elista_kasema_ila_Sio_sheria 🙋🏻‍♂




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz