*JINSI YA KUFURAHISHA MWANAMKE MKIWA KWENYE 6 KWA 6* - EDUSPORTSTZ

Latest

*JINSI YA KUFURAHISHA MWANAMKE MKIWA KWENYE 6 KWA 6*

WATU wengi (hasa baadhi ya wanaume/Wanawake) ama hawajui au hawajali ni kitu gani wenza/mwenza wake anataka kufanyiwa au akifanyiwa kitamsisimua (Turn on) hata kama amechoka sana.
Uchunguzi unaonyesha kuwa Wanaume/wanawake wengi hasa kutoka nchi za Kiafrika hujali zaidi kumaliza hamu zao za mwili na kamwe hawajali kama wenza/Mwenza wake yuko tayari au la!.
Mf: Inasemekama baadhi ya Wanaume wa Kiafrika ambao ni wakubwa kiumri (wa zamani), au wale ambao wanathamini sana jadi zao asilia ndani ya Afrika, kitu cha kwanza watakacho kuambia mkiwa chumbani ni "njoo hapa" au "vua nguo basi" na kisha utavamiwa kabla hata wewe mwenyewe hujawa tayari na unalazwa chini kama sio unawekewa uume mbele ya uso wako.......halafu watu mnashangaa kuambiwa "mume wangu alinibaka".
Mfano huo unaonyesha ni kwa jinsi gani baadhi ya wanaume wanavyojipendelea(wabinafsi), na mara zote huweka akilini mwao kuwa wanawake/mwanamke ni chombo cha kumridhisha / kumstarehesha/ kumfurahisha na kumliwaza yeye "mwanaume".
Napenda kusema kuwa mwanamke kama mwanadamu pia anahaki ya kuridhishwa, kustareheshwa, kufurahishwa na kuliwazwa pia.
Dhana hiyo potofu imepelekea baadhi ya makabila kuendeleza mila za kuwakusanya wasichana ktk umri wa kuvunja ungo (mwali) na kuwafundisha jinsi ya kuwaridhisha mwanaume kimapenzi " hao wana bahati".
Lakini kwa wale ambao hawafuati/hawana/hawazijui mila hizo wamekuwa wakifuatilia kwa makini na kuamini kila kinachoonyeshwa kwenye "Video" ailimradi tu kiwe kinahusu jinsi ya kumridhisha mwanaume kimapenzi.
Ninavyofahamu mimi ni kuwa , ujuzi, utundu katika kufanya mapenzi inapaswa upate mwalimu mzuri na juhudi zako binafsi kama vile
-ubunifu wako,
-kujaribu,
-kuujua mwili wako na wa mpenzi wako,(ntafundisha somo lijalo)
-ufurahiaji wa mwili wako,
-kujiamini kwako,
-uwazi na ushirikiano wa mpenzi wako.
Ni vema jadi ikabadilishwa na swala zima la kufundishwa/fundwa liwe kwa jinsia zote mbili. Wake kwa waume wafundishe jinsi ya kuridhishana, jinsi ya kufurahia na yale mambo muhimu ya mahusiano ya kimapenzi iwe ni ndoa au mahusiano ya kudumu nje ya ndoa.
Pia ni vizuri utambue kuwa unapoamua kufanya tendo la Ndoa au Ngono ni vyema ukajua mahitaji ya mwenzio iwe mwanaume/mwanamke, jaribu kufamnyia Mwenza wako kitu/vitu tofauti na alivyokuwa akitarajia/alivyozoea ni vizuri zaidi na kutamfanya aendelee kuwa na hamu ya kuwa na wewe kwa muda mrefu "usipigwe kibuti" kwa vile unamjulia.....yaani unajua vipele vilipo na unavikuna vilivyo.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz