‛MPENZI′ WA DIAMOND HALI MBAYA KIAFYA - EDUSPORTSTZ

Latest

‛MPENZI′ WA DIAMOND HALI MBAYA KIAFYA


Hawa ilibainika kwamba ametopea katika ulevi wa pombe kali lakini alisaidiwa na kuacha
PICHANI:Hawa Hassan akiwa na Diamond katika picha ya video ya wimbo wa Nitarejea
 Nitarejea ni moja ya nyimboi ambazo zilitikisa vilivyo na kumtambulisha Zaidi mwanamuziuki Diamond Platnum ukiachilia vibao vingine kama Kamwambie na Mbagala.Wimbo huo uliokuwa kwenye mahadhi ya Zuku ulikutanisha vichwa matata viwili,Diamond na Hawa.

Ukiachilia mbali wimbo huo lakini pia stori kubwa ilikuwa ni mahusiano ya Diamond na Hawa,ikielezwa kwamba walikuwa wapenzi wa muda mrefu tangia kipindi Diamond akiwa anauza mitumba maeneo ya Tandale,hivyo watu walianza kuwatupia macho kwa karibu lakini ghafla penzi hilo lilikufaa Mwanadada Hawa kupotea masikioni na machoni mwa wapenda burudani.
Watangazaji Soud Brown na Kwisa wanaoendesha kipindi cha Shilawadu kupitia Clouds Tv waliwahi kumtembelea msanii huyo Hawa Hassan mara ya kwanza baada ya ripoti kuzagaa ya kwamba msanii huyo ametopea katika matumizi ya vilevi hasa pombe za kienyeji(Gongo ikiwemo) na kufanya naye mazungumzo ambapo msanii huyo alikiri kutumia Gongo.Baada ya mazungumzo hayo Hawa alipata msaada na kufanikiwa kuacha kabisa ulevi ikiwa ni pamoja na kuu nganishwa na Pilli Missana Sober House.

Lakini imeelezwa kwamba hali yake imekuwa mbaya tena na ikizidi baada ya kupata tatizo la Ini ikielezwa kwamba yawezekana ni kutokana na Ulevi.

Kupitia ukurasa wa Shilawadu,Soud Brown aliandika;
“Dah... Nimemtembelea Dada Yetu Msanii Hawa Kusema Kweli Hali Yake Mbaya, Tumbo Lake Kubwa Kama Ana Ujauzito wa Miezi 9 Kasoro, Ana tatzo la Ini, mwili unajaa maji na inabd mara kwa mara akatolewe Maji gharama ni kubwa mno kwa familia Yao”
Aliendelea kueleza tena;

“Hii ni mara ya Tatu Shilawadu Wanakutana Na Hawa, Mara Ya Kwanza Mwaka Jana Ambapo Tulimkuta Akiwa Amebobea Kwenye matumizi Ya Uraibu Aina Ya Gongo, Baada ya mazungumzo Hawa akakubaliana na sisi kuwa Yupo Tayari.Kuachana na Matumizi hayo tukamuunganisha na pillimissanah_sober_house  Akasaidiwa kuacha na akaacha kabisa, Bahati mbaya Baadae Ameanza kusumbuliwa na Ini (Huenda liliathiriwa na uraibu ule) Sasa Hv Hawa anaumwa Sana, Halali ucku Mbavu zinamuuma”
Katika taarifa yake hiyo kwa Umma wa Watanzania mtangazaji huyo alimalizia kwa kuandika; 

“Dada Pili Misana Pamoja na Familia Ya Hawa wanapambana ili kuinusuru Afya Ya Hawa, Watanzania, Wasanii Wenzake Na Wote mnaopata Taarifa hizi Tunawasihi na Tunajisihi Tumshike Mkono Hawa...  
Kutoa Ni Moyo Sio Utajiri, Namba Ya Mama a Hawa Ni +255 762 31 35 87






Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz