KUMBE NA KICHUYA YUMO!! - EDUSPORTSTZ

Latest

KUMBE NA KICHUYA YUMO!!

SHIZA KICHUYA
Wakati michuano ya SportPesa Super Cup ikianza kurindima leo Kenya, uongozi wa Simba kupitia Kaimu Rais wake, Salim Abdallah 'Try Again' umesema kuwa wachezaji watatu wataondoka leo nchini humo.

Tyr Again ameeleza kuwa wachezaji hao watatu ambapo wawili ameficha majina yao, wataondoka kwenda kukipa nguvu kikosi hicho huku mmoja wao akiwa ni Shiza Kichuya.

Simba itaanza kutupa karata yake ya kwanza siku ya Jumatatu dhidi ya Kariobang Sharks kuanzia mida ya saa 9 mchana.

Wakati huyo Yanga inaanza kibarua chake leo kwa kukipiga na Kakamega ikifungua rasmi pazia la michuano hiyo kuanzia saa 7 kamili za mchana.

Mshindi wa kombe hilo ataenda England kukipiga na Everton katika Dimba la Goodson Park.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz