IFAHAMU TUZO ALIYOINASA MESS LEO - EDUSPORTSTZ

Latest

IFAHAMU TUZO ALIYOINASA MESS LEO

LIONEL MESSI

Nyota wa Barcelona na Timu ya Taifa ya Argentina, Lionel Messi ‘L0a Pulga’ ametangazwa kuwa mshindi wa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya soka ya Hispania ‘La Liga’, kwa mwezi Aprili.

Messi ambaye anaongoza kwa mabao kwenye ligi hiyo msimu huu ametangazwa mshindi leo Mei 18, 2018 asubuhi na bodi ya La Liga.

Katika mwezi Aprili, Messi amecheza Mechi 4 na kufunga mabao 6 huku akipiga ‘hat-trick’ mbili dhidi ya Leganes na Deportivo La Coruna ambazo zilimfanya kuongeza idadi ya mabao akimwacha hasimu wake, nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo.

Aprili, Barca imeshinda bao 3-1 dhidi ya Leganes, 2-1 dhidi ya Valencia, sare ya 2-2 dhidi ya Celta Vigo na 4-2 dhidi ya Deportivo La Coruna, mechi ambayo iliwahakikishia ubingwa wa La Liga msimu wa huu.

Messi atakabidhiwa tuzo hiyo kwenye mechi ya Jumapili dhidi ya Real Sociedad kwenye Uwanja wa Camp Nou. Mechi hiyo ni ya mwisho kwa La Liga msimu huu ambapo Barcelona watamuaga nahodha wao Andres Iniesta ambaye anamalizia msimu na kuondoka Klabuni hapo.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:

Delivered by EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz