HABARI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO MAY 28,2018 - EDUSPORTSTZ

Latest

HABARI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO MAY 28,2018

mpira wa miguu

Manchester City wanamtaka Kylian Mbappe ikiwa Paris St-Germain watashindwa kumchukua
Manchester City iko tayari kukamilisha mipango ya Kylian Mbappe ikiwa vikwazo vya kifedha vya fair play vitawalazimisha Paris St-Germain kuacha mpango wao kukamilisha mkataba na mshambuliaji huyo Mfaransa mwenye umri wa 19, ambaye alichukua mkopo kutoka Monaco mwaka mmoja uliopita . (Manchester Evening News)

RB LeipzigWako tayari kumchukua winga wa Everton Ademola Lookman baada ya kijana huyo mwenye umri wa miaka 20-kufanikiwa kumaliza deni lake nchini Ujerumani . (Liverpool Echo)

Mchezaji wa safu ya ulinzi wa timu ya Freiburg Caglar Soyuncu, mwenye umri wa miaka 22, anasisitiza kuwa hana mkataba kwa sasa na Arsenal lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Uturuki anataka kufanya mazungumzo naklabu hiyo. (Goal)
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester United Paul Pogba amedai kurejea Juventus
Fulham ambao walipandishwa daraja wanasemekana wanataka kumchukua mchezaji wa kiungo cha kati wa timu ya Auxerre Lamine Fomba. (L'Equipe - in French)

Chelsea huenda wakahitaji kuongeza mara dufu pesa kiasi cha Euro £3.5m ikiwa wanamtaka Maurizio Sarri, ambaye aliondoka Napoli Jumatano iliyopita,kuchukua nafasi ya Antonio Conte kama kocha. (Corriere dello Serra via Sun)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa The Blues mwenye umri wa miaka 27 Mfaransa N'Golo Kante, ambaye amekuwa akipigiwa upatu kuhamia na Paris St-Germain, anasema kwamba huku akipenda kuishi mjini London, moyo wake utasalia Paris. (Star)


N'Golo Kante huenda akahamia Paris St-Germain japo moyo wake utasalia kuwa London
Inter Milan wamepanga kukutana na mshambuliaji Mauro Icardi, mwenye umri wa miaka 25, katika kipindi cha wiki ijayo kujadili mpango wa kumuongezea mkataba. (Football Italia)

Liverpool wako tayari kumtafuta mlinda lango huku mchezaji wa Roma Mbrazil Alisson, mwenye umri wa miaka 25, na Mslovania Jan Oblak mwenye umri wa miaka 25 anayechezea Atletico Madrid wakiwa miongoni mwa wanaolengwa na Liverpool. (Mirror)

The Reds wanafuatilia kwa makini mlinda lango kijana chipukizi wa AC Milan Mtaliano Gianluigi Donnarumma, 19. (La Repubblica - in Italian)

Manchester United tayari wako tayari kumnunua Gareth Bale wa Real Madrid kwa milioni £, lakini ana hofu juu ya mtindo wa mchezo wa Jose. (Sun)

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, mwenye umri wa miaka 33, anajiandaa kurejea Manchester United
Kijana kutoka Wales , 28, anasema uamuzi wake ikiwa ataondoka Madrid huku Bayern Munich pia ikitaka kusaini nae mkataba . (Telegraph)

Hata hivyo huenda Bale asihamie Manchester City huku mabingwa hao wa Ligi ya Primia wakionekana kutokuwa na haja ya kusaini mkataba na mchezaji huyo wa kiungo cha kati. (Guardian)

Mo Salah: Nina 'matumaini makubwa' ya kucheza Kombe la Dunia
Meneja wa Bale, Zinedine Zidane hakuzungumza na mchezaji huyo kwa zaidi ya saa nne baada ya fainali ya ushindi wa Ligi ya dhidi ya Liverpool. (Star)

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, mwenye umri wa miaka 33, anajiandaa kurejea Manchester United. (Diario Gol via Express)

Manchester United wamewasilisha ombi la thamani ya Euro milioni £96m la kumnunua mchezaji wa timu ya Lazio anayecheza safu ya kati Mserbia Sergej Milinkovic-Savic, mwenye umri wa miaka 23. (Metro)
Bale asihamie Manchester City Zinedine Zidane hakuonyesha kumg'ang'ania Bale , licha ya kwamba timu nyingine zinamtaka
Mchezaji wa safu ya mashambulizi ya Lyon na mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Nabil Fekir, mwenye umri wa miaka 24, anasema ''hajakaribia'' kuhamia Liverpool na atachukua muda kufikiria juu ya hali yake . (Telefoot via Sky Sports)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester United Paul Pogba amedai kurejea Juventus. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 raia wa Ufaransa alikuwa miaka minne na championi ya Serie A baada ya kuhamia Italia kutoka Old Trafford mwaka 2012. (Tuttosport via Express)

Real Betis wameanza mazungumzo na ManchesterUnited kuhusiana na uwezekano wa Mbrazil Andreas Pereira, mwenye umri wa miaka 22 anayecheza safu ya kati kucheza kwa deni katika kikosi cha uhispania katika timu za Granada na Valencia. (Mirror)

Liverpool iko tayari kurefusha zaidi mkataba wa mchezaji wa England wa safu ya kati - nyuma Joe Gomez kuongeza mkataba
Mshambuliaji wa Roma Edin Dzeko sanasema kuwa aliambiwa aikatae Chelseawakati wa msimu wa kuhama uliopita. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Bosnia mwenye umri wa miaka 32, aliongeza kuwa atakua tayari kwa uhamisho kutoka katika mji mkuu wa Italia msimu huu . (Face TV via Sun)

Inter Milan wamepanga kukutana na mshambuliaji Mauro Icardi, mwenye umri wa miaka 25, katika kipindi cha wiki moja ijayo kujadili mkataba mpya kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina. (Football Italia)


Liverpool iko tayari kurefusha zaidi mkataba wa mchezaji wa England wa safu ya kati - nyuma Joe Gomez kuongeza mkataba , licha ya kwamba kijana huyo mwenye umri wa miaka 21 bado ana miaka minne yya kuendelea kutumikia mkataba wake katika Anfield. (Sun)

mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester United Scott McTominay, mwenye umri wa miaka 21, ameahidi kuchezea Uskochi siku zijazo , akisema hakuna "nafasi" kwake ya kuichezea England . (Mail)

Mlinzi wa Aston Villa John Terry, 37,ataondoka kwenye klabu hiyo msimu huu baada ya upande wa Steve Bruce kupoteza mchezo wa fainali wa Champion Ligi . (Sun)



EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz