STORY ZA USAJILI BARANI ULAYA - EDUSPORTSTZ

Latest

STORY ZA USAJILI BARANI ULAYA




Na George Mganga

Taarifa zinaeleza kuwa Golikipa namba moja wa timu ya Taifa ya Spain na Manchester United, David de Gea (27) anatajwa kuongeza mkataba mwingine wa kuitumikia timu hiyo, hivyo ataondoa uvumi mwingine wa kuelekea Real Madrid. (Times)

Mabingwa mara mbili mfululizo wa UEFA Champions League, Real Madrid, wapo katika mchakato wa kufanya mazungumzo na winga wa Manchester City, Raheem Sterling (23) ambaye anamaliza mkataba wake 2020. Inaelezwa bado hajaanza mazungumzo yoyote ya kuongeza mkataba na timu hiyo. (Mirror)

Tetesi zinasema pia Real Madrid ipo tayari kumuchia mshambuliaji wake kutoka Wales, Gareth Bale (28), katika msimu huu wa majira ya joto. (Independent)

Chelsea ipo kwenye mazungumzo na Nahodha wa Newcastle United, Jamaa Lascelles, ili aje kuimarisha nafasi ya ulinzi katika kikosi chao msimu ujao. (Evening Standard)

Kibibi kizee cha Torino, Juventus FC, wamefikia makubaliano na beki wa kushoto wa Manchester United, Matteo Darmian (28), ili aende kuitumikia timu hiyo. (Calciomercato - Italy)

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz