UZINDUZI WA KAMPENI YA MAANDALIZI YAKOMBE LADUNIA MOROCCO - EDUSPORTSTZ

Latest

UZINDUZI WA KAMPENI YA MAANDALIZI YAKOMBE LADUNIA MOROCCO

Image captionMorocco imezindua kampeni yake ya kuandaa mashindano ya kombe la dunia ya 2026 mjini Casablanca.

Morocco imezindua kampeni yake ya kuandaa mashindano ya kombe la dunia ya 2026 mjini Casablanca.

Taifa hilo la Afrika kaskazini ambalo limewasilisha ombi lake la tano kuandaa fainali hizo , linakabiliwa na ushindani mkali kutoka ombi la pamoja linaloshirikisha Canada, Mexico na Marekani.

Mwenyekiti wa ombi hilo Moulay hafid Elalamy amesema kuwa Morocco itaonyesha mchezo mzuri zaidi, katika kombe hilo la dunia.

Uamuzi wa ni nani atakayeandaa kombe hilo utafanywa tarehe 13 Juni , mkesha wa kombe la dunia la mwaka 2018 mjini Moscow.

''Tunaahidi kuonyesha mchuano mzuri na kusheherekea thamani ya Umoja na amani'', aliongezea Elalamy.

''Maandalizi ya kombe la dunia nchini Morocco yataleta ufanisi wa kibiashara na kuwacha historia kubwa, na iwapo tutashinda heshima ya kuandaa dimba hilo tunaamini kwamba mshindi atakuwa soka, vijana wa taifa letu ,Afrika na dunia nzima kwa jumla''.

Hakuna maelezo yaliotolewa kuhusu miji andalizi huku kura ya kubaini atakayeandaa ikiwa umbali wa miezi mitano.

Taifa hilo la Afrika kaskazini limefeli katika maombi yake manne miaka 1994, 1998, 2006 na 2010.

Mwaka wa 2010, mchuano huo uliandaliwa na Afrika Kusini huku bara hili likiandaa kombe hilo kwa mara ya kwanza katika historia.

Morocco inataka kubadili hayo yote na imemteua Elalamy, waziri wa serikali, kuongoza ombi hilo huku aliyekuwa katibu mkuu wa shirikisho la soka Afrika Hicham El Amrani akiwa afisa mkuu mtendaji.
NDG MSOMAJI WA EDUSPORTSTZ UNAKUMBUSHWA KUSUBSCRIBE NA KUFOLLOW WEB YETU PAMOJA NA MITANDAO YETU YA KIJAMII CHINI YA POSITI HII ILI KUTUMIWA UPDATES ZOTE ZA AJIRA, MICHEZO, HABARI, SCHOLARSHIPS PAMOJA NA MASTORI YA MASTAA NA VIONGOZI MBALIMBALI. EDUSPOTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI.
EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati. BOFYA HAPA KUJIUNGA NA INNOVATION FURSA CHALLENGE http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
UNGANA NASI KUPITIA LIKI HIZI ILI KUTUMIWA HABARI POPOTE ULIPO

EDUSPORTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI

WEKA EMAIL YAKO:


Delivered by EDUSPOTSTZ
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz