MASHABIKI WA YANGA WAIBUA MASWALI LUKUKI KUHUSU CHIRWA - EDUSPORTSTZ

Latest

MASHABIKI WA YANGA WAIBUA MASWALI LUKUKI KUHUSU CHIRWA

RUNGU LA TFF HALIJAMWACHA CHIRWA SALAMA
MZAMBIA Obrey Chirwa amekaa nje ya kikosi cha Yanga kwa zaidi ya wiki mbili kwa kuwa alikuwa na mgomo akitaka kulipwa fedha zake za usajili ambazo Klabu ya Yanga ilishindwa kutimiza kwa wakati kama walivyokubaliana.



Baada ya kurejea kwao Zambia akiwa ameomba ruhusa, siku za kurejea zilipowadia, Chirwa aligoma kurudi akishinikiza alipwe fedha zake la sivyo asingerudi.


Pamoja na kwamba uongozi wa Yanga ulifanya juhudi kubwa kutaka kulifukia suala hilo, baadaye ukweli ulijulikana kwamba Chirwa ameamua kubaki Zambia akijihusisha na kilimo hadi hapo atakapolipwa.

Kurejea kwake, ingawa imekuwa siri, inaonyesha atakuwa amelipwa angalau kiasi fulani. Nakukumbusha, lazima kuna wachezaji ndani ya Yanga ambao watakuwa wanadai lakini waliendelea kubaki na kuitumikia timu hiyo.




Chirwa ana haki ya kudai na lazima tukubali hili. Tukirudi kwenye msingi wa msimamo wake, lazima tutakuwa na maswali ambayo nimewahi kuuliza na leo nitaongeza kadhaa ili kupata majibu.




Kwamba, kama aligoma kwa wiki mbili na ushee, Yanga ilikuwa na majukumu kadhaa kama yale ya Kombe la Shirikisho, ligi na Kombe la Mapinduzi. Akishalipwa fedha alizokuwa anadai, mwisho wa mwezi atachukua mshahara wakati hakuwa akiitumikia Yanga?




Pili; Wakati kuna wengine wanadai na walibaki wakaendelea kuipigania Yanga, kurejea kwake na siku moja tu akapelekwa Zanzibar na kujiunga na timu, viongozi hawaoni wameonyesha udhaifu kwa kuwa wanawavunja nguvu wengine waliobaki?




Sasa nakuja katika hili, amerudi wenzake wakiwa nusu fainali, wanapigania kwenda fainali. Moja kwa moja kapata nafasi ya kukaa benchi na mwisho amepiga penalti ya mwisho ambayo inaiondoa Yanga. Tunaweza kusema ni mambo ya mpira lakini nani mwisho amekosea na kuitoa timu?


Jibu ni Chirwa na kama atasamehewa hiyo ndiyo maana ya mchezo na kujenga kukubali masuala ya kiuanadamu kwamba kila mmoja wetu anakosea na ukitaka kuishi na watu vizuri, basi lazima ukubali makosa yao pia. Au nifupishe, uvumilivu unaweza kuwa dawa zaidi ya muarobaini.


Juhudi za wenzake wote zimeishia mguuni mwake. Waliziba pengo lake na kumpigania lakini amerejea ameonyesha si mtu makini. Na kama utasema kukosa penalti ni jambo la kawaida na Yanga wanapaswa kuelewa na kumvumilia, mimi nitakuuliza vipi yeye alishindwa kuwavumilia?


Unakumbuka Portsmouth ya England, wachezaji wake waliipigania timu bila mishahara tena hiyo ni England, walifanya hivyo hadi mwisho wao. Leo Chirwa anaonyesha jeuri na mwisho anarejea na kupewa nafasi haraka, halafu mwisho anakosea na kosa lake linaitoa timu mashindanoni!





Viongozi Yanga, wanapaswa kuwa makini na kuangalia mambo yanayohusisha saikolojia ya wachezaji wao. Wanapaswa kupima mambo kabla ya kufanya na lazima wajue kama viongozi hawapaswi kuwa waoga na wao ndiyo wanaopaswa kusimamia nidhamu na kuwaonyesha wachezaji kama Chirwa na wengine wanaojiona ni wakubwa kuliko klabu kuwa lazima washikilie nidhamu, ambaye atakuwa hataki, abebe mabegi yake aende na Yanga itatumikiwa na wengine na itafanikiwa. Ndiyo maana ilifika nusu fainali bila ya Chirwa, Donald Ngoma na wengine.


Viongozi, acheni uoga, acheni kupapatikia wachezaji wageni au wale wanaoonekana walifanya vizuri kwa kuwa hilo ndiyo jukumu lao, hawaisaidii Yanga.


EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati. BOFYA HAPA KUJIUNGA NA INNOVATION FURSA CHALLENGE http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
UNGANA NASI KUPITIA LIKI HIZI ILI KUTUMIWA HABARI POPOTE ULIPO


EDUSPORTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI

WEKA EMAIL YAKO:


Delivered by EDUSPOTSTZ
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz