MAN U KUWEKA DONGE LA KUFURU KWA NEYMAR KUIPIKU PSG - EDUSPORTSTZ

Latest

MAN U KUWEKA DONGE LA KUFURU KWA NEYMAR KUIPIKU PSG



Imeripotiwa kuwa Manchester United wameamua kutoa dau la £444m kwa ajili ya nyota wa Paris Saint-Germain Neymar.


Wakati wa majira ya joto, Neymar alihama kwa dau la rekodi ya dunia kutoka Barcelona kwenda Parc des Princes, na Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazili amefunga magoli 20 katika mechi 22 za michuano yote.

Hata hivyo hofu imezuka kuhusu furaha ya mchezaji huyo mwenye miaka 25 katika Ufaransa na Real Madrid inaaminika kuwa tayari kutoa dau nono kumsajili mchezaji huyo ikiwa atakuwa sokoni miezi 18 ijayo.

Miamba wa La Liga hata hivyo wanaweza kukabiliwa na ushindani kutoka kwa United, kwani miamba hao wa Uingereza wanajiandaa kutoa dau la £444m kwa ajili ya mchezaji huyo, kwa mujibu wa Le 10 Sport.

Ofa hiyo itaipita kwa mbali £365m ambayo inaaminika Madrid walitaka kutoa kwa ajili ya nyota huyo, kwani United watakuwa na wepesi wa kuzungumza.

Mkataba wa Neymar na vinara hao wa Ligue 1 unafika kikomo 2022.
Facebook CommentsEDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.

BOFYA HAPA KUJIUNGA NA INNOVATION FURSA CHALLENGE http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
UNGANA NASI KUPITIA LIKI HIZI ILI KUTUMIWA HABARI POPOTE ULIPO

EDUSPORTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI

WEKA EMAIL YAKO:


Delivered by EDUSPOTSTZ
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz