YANNICK BOLLASIIE ARUDI RASMI MAZOEZINI - EDUSPORTSTZ

Latest

YANNICK BOLLASIIE ARUDI RASMI MAZOEZINI


Mshambuliaji wa Everton Yannick Bolasie amerudi katika mazoezi baada ya miezi 11 akiuguza jeraha

Mshambuliaji wa Everton Yannick Bolasie amerudi katika mazoezi baada ya miezi 11 akiuguza jeraha.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 alipata jeraha baya wakati klabu yake ilipotoka sare ya 1-1 dhidi ya Manchester United mnamo mwezi Disemba 4, 2016 na hadi kufikia sasa amefanyiwa upasuaji mara mbili.

Raia huyo wa DR Congo alifanya mazoezi na timu ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 23 wiki iliopita kabla ya kujiunga na kikosi kikuu siku ya Jumatano.

Klabu hiyo imesema kuwa alipokea pongezi kutoka kwa wachezaji wenza baada ya kurudi.

Bolasie ameichezea klabu hiyo mara 15 tangu ahamie kutoka Crystal palace 2016.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz