HANS POPPE:SISI HATUWEZI KUENDELEA KUMLIPA MTU AMBAYE HACHEZI - EDUSPORTSTZ

Latest

HANS POPPE:SISI HATUWEZI KUENDELEA KUMLIPA MTU AMBAYE HACHEZI






Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema beki wao Shomari Kapombe anatakiwa kuanza kucheza la sivyo anaweza kwenda.


Hans Poppe amesema Simba haiwezi kuendelea kumlipa mchezaji ambaye hawatumikii.


“Vipimo vinaonyesha Kapombe amepona, vizuri akaanza kucheza. Hata sisi hatuwezi kuendelea kumlipa mtu ambaye hachezi.


“Sasa tunamuachia yeye, arejee acheze au kama vipi basi aende akajiuguze hadi atakapopona,” alisema Hans Poppe.


Kapombe ameendelea kuwa nje ya uwanja tokea amejiunga na Simba akitokea Azam FC.

Beki huyo wa zamani wa Simba amekuwa akiendelea kujitibia kutokana na majeraha yake.




Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz