MATUKIO YA PICHA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM KATA YA KIJICHI - EDUSPORTSTZ

Latest

MATUKIO YA PICHA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM KATA YA KIJICHI



Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe akimnadi mgombea wa CCM katika uchaguzi wa marudio wa Udiwani Kata ya Kijichi, Eliasa Mtalawanje,Temeke Dar es Salaam, leo. Akizungumza amesema CCM itashinda Udiwani kata zote tatu ambako uchaguzi unarudiwa mkoani Dar es Salaam. Kata zingine ni Saranga na Mbweni.


Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe akiwasili kwenye Uwanja wa mkutano kuzindua kampeni za Uchaguzi mdogo wa Udiwani kata ya Kijichi, leo. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Temeke Almishi Hazal


Wananchi na wana CCM wakishangilia wakati Kusilawe na viongozi wenzake wakiingia Uwanjani


Vijana wa hamasa wakichangamsha mkutano huo


Madansa wakicheza muziki kuchangamsha mkutano huo wa uzinduzi wa kampeni za CCM za Udiwani kata ya Kijichi.


Mgombea Udiwani kwa tiketi ya CCM kata ya Kijichi Eliasa Mtalawanje akisalimia baada ya kutambulishwa kutambulishwa kwenye mkutano huo


Mtalawanje akitroti baada ya kutambulishwa na Mwenyekiti wa Wazee wa CCM Temeke


Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CCM Wilaya ya Temeke Mohammed Mbonde, akizungumza baada ya kukaribishwa jukwaani kusalimia.


Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Wilaya ya Temeke Mohammed Mbonde, akipongezwa na Mgombea Udiwani kata ya Kijichi Eliasa Mtalawanje baada ya kutoka jukwaani kusalimia.


Meya wa Temeke Abdallah Chaurembo akisalimia wananchi kwenye mkutano huo, na kuzungumza kuhusu umuhimu wa wananchi kumchagua mgombea wa CCM Udiwani kata ya Kijichi.


Mbunge wa Mbagala Issa Mangungu, akisalimia wananchi kwenye mkutano huo, na kuzungumza kuhusu umuhimu wa wananchi kumchagua mgombea wa CCM Udiwani kata ya Kijichi.


Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Temeke Almishi Hazal akisalimia wananchi na kumkaribisha Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, kuhutubia mkutano huo na kumtambulisha mgombea wa CCM wa Udiwani Kata ya Kijichi


Vijana wa hamasa na wananchi wakiwa wametulia kumsikiliza


Baadhi ya wananchi kwenye mkutano huo


Viongozi wa Barza la wazee Temeke wakiwa kwenye mkutano huo


Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Saad Kusilawe akihutubia mkutano huo


Kusilawe akisisitiza jambo


Vijana wa CCM wakimshangilia Kusilawe


Msimamizi wa uchaguzi wa CCM makao makuu Mzee Kazidi (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa Wilaya ya Temeke Almishi Hazal. katikati ni Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam


Mzee Kazidi akizungumza kwenye mkutano huo. Kulia ni Kuslawe.


Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe akimnadi mgombea wa CCM katika uchaguzi wa marudio wa Udiwani Kata ya Kijichi, Eliasa Mtalawanje,Temeke Dar es Salaam, leo


Kisha akamkabidhi mgombea huyo ilani ya CCM


Kusilawe akimkabidhi ilani mgombea huyo


Mgombea akionyesha ilani baada ya kukabidhiwa


Mgombea wa CCM katika uchaguzi wa marudio wa Udiwani Kata ya Kijichi, Eliasa Mtalawanje,Temeke Dar es Salaam, akizungumza na kuomba kura baada ya kunadiwa na Kusilawe, leo


Eliasa Mtalawanje akifafanua jambo kwa makini


Wananchi wakimshangilia mgombea huyo


Mgombea huyo akiendelea kuomba kura kwa wananchi


Mgombea wa CCM katika uchaguzi wa marudio wa Udiwani Kata ya Kijichi, Eliasa Mtalawanje,Temeke Dar es Salaam, akiondoka uwanjani mwishoni mwa mkutano. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

 like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika Propellerads

For Booking>>>



CALL>>>

Voda: +255757441463

JIUNGE NAMI KUPITIA LINK HIZI










Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz