TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA SIKU YA LEO - EDUSPORTSTZ

Latest

TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA SIKU YA LEO


 Alex Oxlade-Chamberlain, wakitaka kuwapiku Chelsea. (Mirror)

Liverpool watajaribu kwa mara ya mwisho kutaka kumsajili Alex Oxlade-Chamberlain, wakitaka kuwapiku Chelsea. (Mirror)

Paris Saint Germain wamekataa dau la pauni milioni 32.4 kutoka kwa Barcelona kumtaka Angel Di Maria, 29. (AS)

Barcelona bado wanataka kumsajili Philippe Coutinho na Angel Di Maria, baada ya kukamilisha usajili wa Ousmane Dembele. (Marca)

Inter Milan inataka kuwasajili Shkodran Mustafi, 25, wa Arsenal na Eliaquim Mangala, 26, wa Manchester City. (Gazzetta dello Sport)


Manchester City na Paris Saint-Germain zitapambana kumsajili kiungo wa Porto Danilo Pereira. (A Bola)

Calgliari wanataka kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Loic Remy. (Sky Sport Italia)

Marseille wanafikiria kumtaka mshambuliaji wa Liverpool Divock Origi, baada ya Olivier Giroud kuamua kubakia Emirates. (Mercato)
Tottenham wanajaribu kukamilisha usajili wa beki wa kimataifa wa Ivory Coast Serge Aurier, 24, kwa pauni milioni 23 kutoka Paris Saint-Germain kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Guardian)

Paris Saint-Germain wamekamilisha makubaliano na Monaco ya kumsajili Kylian Mbappe, 18, na kiungo mkabaji Fabinho, 23, kutoka Monaco. (Daily Record)

Chelsea wanapanga kuwa na mazungumzo na Everton kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 30 wa kiungo Ross Barkley baada ya timu hizo mbili kucheza siku ya Jumapili. (Sun)

Chelsea pia wanafikiria kupanda dau la kumtaka mshambuliaji wa Swansea Fernando Llorente, 32 ambaye anataka kucheza tena chini ya Antonio Conte. (Daily Telegraph)

Arsenal watamuuza beki Shkodran Mustafi, 25, kabla ya dirisha la usajili kufungwa iwapo watapata dau la pauni milioni 35, ambazo walilipa kumnunua kutoka Valencia mwaka jana. Juventus na Inter Milan zinamtaka beki huyo. (Daily Mail)

Meneja wa West Brom Tony Pulis yuko tayari kupanda dau la pauni milioni 30 kumsajili beki wa Liverpool Mamadou Sakho, 27. (Daily Telegraph)

Crystal Palace wana uhakika wa kumsajili Mamadou Sakho aliyecheza kwa mkopo katika klabu hiyo msimu uliopita. (Times)

Newcastle na Watford zinafikiria kumsajili mshambuliaji wa Leicester City Islam Slimani, 29. (Daily Mirror)

Arsenal huenda wakapanda dau kumtaka mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzima, 29, iwapo Alexis Sanchez ataondoka Emirates. (Diario Gol)

Arsenal wapo tayari kumuuza Alex Oxlade Chamberlain, 24, kwa timu itakayopanda dau la pauni milioni 35, huku Liverpool na Chelsea zikimtaka. (Daily Mirror)


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz