SIMBA MLICHOKIFUATA SAUZ KIDHIHIRISHENI NYUMBANI - EDUSPORTSTZ

Latest

SIMBA MLICHOKIFUATA SAUZ KIDHIHIRISHENI NYUMBANI




Kikosi cha Simba, kilikwenda Afrika Kusini.

KIKOSI cha Simba, kilikwenda Afrika Kusini kuweka kambi ya ku­jiandaa na msimu ujao ambapo wikiendi hii kinatarajiwa kurejea nchi­ni tayari kwa tamasha lao la kila mwaka la Simba Day.

Simba ilikwenda nchini humo Julai 17, mwaka huu ikiwa na wachezaji wachache kutokana na wengine kuwa na majukumu na timu ya taifa.

Baada ya kupita wiki kad­haa, kikosi chao kikakamilika huko Sauz, hali iliyowafanya benchi lao la ufundi chini ya Kocha Mkuu, Joseph Omog raia wa Cameroon kuona wapi kuna upungufu ili aufanyie kazi mapema kabla ya kuanza kwa msimu.

Ikumbukwe kuwa, Simba wakiwa huko, waliendelea ku­fanya usajili wa wachezaji kad­haa ambapo nao walipoungana na wenzao, kikaonekana kikosi kimekamilika.


Katika wiki yao ya mwisho, wakacheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Orlando Pirates na Bidvest Wits. Hizo zote zina­shiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini.

Katika mchezo wa kwanza, Simba ilikubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Orlando Pirates, kisha mchezo uliofuata ikalaz­imishwa sare ya kufungana bao 1-1.


Najua wazo la kwenda ku­weka kambi nje ya nchi lilikuwa na maana kubwa kwa sababu benchi la ufundi kuna kitu li­likuwa linataka kuwapa wache­zaji wake, hivyo imani yangu ni kwamba wamekipata hicho kitu.

Kama tujuavyo, msimu wa 2017/18 utaanza rasmi Agosti 26, mwaka huu baada ya Agosti 23, kupigwa mchezo wa Ngao ya Jamii kuashiria kufunguliwa kwa msimu huo utakaozikutanisha Simba na Yanga.

Wapenzi wengi wa timu ya Simba, wanasubiri kuiona timu yao ikifanya vizuri msimu ujao kutokana na kwamba wa­naamini kambi ya nje ya nchi imekijenga kikosi chao vile wa­navyotaka.


Kabla ya kuanza kwa msimu, watapata fursa ya kuwaona wachezaji wao kwenye mechi dhidi ya Rayon Sport katika Tamasha la Simba Day, Ju­manne ijayo ya Agosti 8, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wachezaji onyesheni uw­ezo wenu na kuwaaminisha mashabiki wenu kwamba msimu ujao mtakuwa moto kia­si gani. Katika Simba Day, cheze­ni soka la uhakika. Mkifanya kinyume na hapo mtawavunja moyo wanaowasapoti.

Mbali na suala hilo la Simba, naamini kila mmoja anafahamu kwamba kesho Jumapili dirisha la usajili linatarajiwa kufungwa, hiyo ni kwa mujibu wa Shirik­isho la Soka Tanzania (TFF) am­bapo dirisha hilo lilifunguliwa Juni 15, mwaka huu.

Naamini kwa siku zote hizo takribani 50, kila timu ime­kirekebisha kikosi chake kwa aji­li ya kufanya vema msimu ujao. Pia hata katika ushiriki wenu wa Kombe la Shirikisho Afrika msimu ujao, mashabiki wata­taka kuona matunda yenu.

Nitashangaa kusikia mpaka dirisha linafungwa, timu fu­lani haijakamilisha usajili wake wakati kulikuwa na siku nyingi za kufanya hivyo.

TFF imekuwa taasisi ya kiung­wana sana kwani ilikuwa ikitoa ukumbusho kwa klabu mbalim­bali kukamilisha usajili wake ili kuepuka adhabu itakayowa­kumba.

Adhabu itakayoikumba timu ambayo itabainika haijakamili­sha usajili wake mpaka dirisha linafungwa, itashushwa ma­daraja matatu. Zoezi hili la usa­jili ambalo linafungwa kesho linazihusisha timu za Ligi Kuu Bara, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili.

Naamini hakuna timu am­bayo itakubali ishushwe daraja kutokana na suala hilo. TFF nayo iwe na msimamo, kama kweli dirisha linafungwa kesho, iwe kesho kweli na isitokee siku zikaongezwa kwa maslahi ya timu fulani ambayo inaonekana ni kubwa hapa nchini.


Nasema hivyo kwa sababu kipindi kilichopita kama hiki, siku zilipoisha, ziliongezwa tena, ikatoa fursa kwa timu zi­lizoshindwa kukamilisha usa­jili wake kumalizia zoezi hilo hali ambayo haikuleta picha nzuri.

Mwisho kabisa nimalizie na Uchaguzi Mkuu wa TFF ambapo Jumamosi ya wiki ijayo ndiyo utafanyika kule Dodoma kama ilivyopangwa hapo awali.

Ni muda muafaka sasa kuan­za kutega masikio na kusikiliza sera za wagombea kwani wiki ijayo ndiyo kampeni zitaanza. Hivyo tusikilize hoja za wago­mbea na kuzichambua vizuri, kisha achaguliwe mtu kulingana na kile ambacho tunaamini ki­takuwa na manufaa kwa soka letu na wala si kwa mtu binafsi.

Tumeona uongozi uliopita jinsi ulivyoliongoza soka letu, japo kulikuwa na mabaya, lakini mazuri nayo yalikuwepo tena mengi tu. Hivyo ni jukumu la viongozi wanaokuja kuongoza kwa weledi.
Niwatakie kila la heri wago­mbea wote, lakini pia niwaombe wajumbe ambao watapiga kura, watuchagulie viongozi bora.


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz