GHARAMA YA DEMBELE KUFIKIA KIWANGO CHA NEYMAR - EDUSPORTSTZ

Latest

GHARAMA YA DEMBELE KUFIKIA KIWANGO CHA NEYMAR

Dembele akifiungia France bao la ushindi dhidi ya Uingereza

Ousmane Dembele ana uwezo wa kuwa kama Neymar na huenda akawa mshindi wa taji la mchezaji bora dunia Ballon d'Or, kulingana na mchezaji wa zamani wa Uingereza na Bayern Munich Owen Hagreaves.


Dembele anatarajiwa kujiunga na Barcelona kwa kitita cha pauni milioni 135.5 kutoka klabu ya Ujerumani ya Borussia Dortmund.

Kiticha hicho cha uhamisho ni cha pili kwa thamani baada ya kile cha pauni milioni 200 ambazo Barca walipokea walipomuuuza Neymar kwa PSG.

Akizungumza kuhusu Dembele, Hagreaves aliambia BBC ni mchezaji bora mwenye umri wa miaka 20 duniani.

Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United aliongezea: Amekuwa akisakwa lakini mtu yeyote ambaye amemuona akicheza nchini Ufaransa na katika ligi ya Bundesliga msimu uliopita atajua kwamba ni mchezaji mzuri sana.

''Atakuwa ndoto dhidi ya mabeki wengi''.

''Kimaumbile ana nguvu na anaweza kucheza kwa kutumia miguu yote miwili.Anaweza kupiga mipira ya adhabu kwa kutumia miguu yote miwili''.


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz