Klabu ya Juventus kutokea nchini Italia,imekua klabu ya kwanza kwa msimu huu kutinga hatua ya fainali ya michuano ya Uefa Champions League baada ya kuilaza AS Monaco goli 2-1 usiku wa kuamkia leo.
Katika ushindi huo magoli ya Juve yalifungwa na Mario Mandzukic mnamo dakika ya 39 kabla ya Dann Alves kupigilia msumali mwingine (goli la 2) magoli yaliyodumu hadi kumalizika kwa kipindi cha kwanza.Monaco walijitahidi kutaka kurehesha magoli na mnamo dakika ya 69 Kylani Mbappe kinda Monaco akaiandikia bao pekee timu yake.
Juve sasa imeingia hatua ya fainali ikwa ni kwa Agrigate ya goli 4-1 kwani katika mchezo wa hatua ya kwanza iliibuka na ushindi wa goli 2-0 na pia hii itakua ndio fainali yake ya pili.
TASWIRA KATIKA PICHA BAADA YA USHINDI WA JUVE..
Hapo chini ni mashabiki wa Juve wakionyesha furaha yao baada ya timu yao kushinda.
No comments:
Post a Comment