BREAKING: HUYU HAPA KOCHA MPYA WA SIMBA

 

Ni rasmi klabu ya Simba imethibitisha kumuajiri Dimitar Pantev raia wa Bulgaria kurithi mikoba iliyoachwa na Fadlu Davids

Pantev anatua Simba kwa mkataba wa miaka miwili akikabidhiwa jukumu la kusimamia malengo ya Simba msimu huu baada ya Fadlu kuondoka

Jukumu namba moja ni kuhakikisha Simba inabeba ubingwa wa ligi kuu na kufanya vyema katika michuano ya ligi ya mabingwa ambapo kazi yake ya kwanza ni kuhakikisha Simba inatinga hatua ya makundi

Pantev anatarajiwa kuanza rasmi majukumu yake siku ya Jumatatu


0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post