Nilikuwa mwanafunzi wa tatu wa sekondari wakati matatizo yangu yalianza. Nilianza kushuka darasani, nilikuwa nakosa masomo na nilipata wito wa wazazi kuja shule mara kwa mara.
Walimu walishasema kuwa kama sitabadilika, nitafukuzwa shule kwa sababu nilionekana kama sifanyi bidii na matokeo yangu yalizidi kuwa mabaya. Niliporudi nyumbani nilipata adhabu za kila mara na wazazi walipoteza matumaini kwangu.
Nilianza kukosa marafiki shuleni kwa sababu kila mtu aliona kama mimi ni tatizo. Nilikuwa nikienda shuleni kwa wasiwasi kila siku nikihofia kuitwa ofisini. Nilipoteza hamu ya kusoma na hata nikiwa darasani nilikuwa na mawazo mengine. Nilijua kabisa maisha yangu yalikuwa yanaenda vibaya na niliona mustakabali wangu unaharibika. Soma zaidi hapa

Post a Comment