Katika kijiji kimoja kilichojaa midomo na minong’ono, tukio lisilo la kawaida liliwasha moto wa mazungumzo miongoni mwa wakazi. Mama mmoja alichukua hatua kali baada ya kunasa binti yake wa kwanza akijaribu kutoroka usiku kujiunga na marafiki zake. Tukio hilo lilishuhudiwa na majirani kadhaa, na kwa muda mfupi likawa gumzo kubwa kijijini humo.
Mashuhuda wanasema kuwa binti huyo alikuwa amepanga kutoka nyumbani akiwa amevalia nguo za kifahari, akipulizia marashi mazito kana kwamba alikuwa akielekea kwenye sherehe kubwa.
Mama yake aliposhtuka baada ya kusikia mlango ukifunguliwa taratibu, aliamua kumfuatilia kimya kimya. Dakika chache baadaye, binti huyo alinaswa mikononi, akishikiliwa na rafiki zake wawili waliokuwa wakimsubiri barabarani. Soma zaidi hapa

Post a Comment