Kuna wakati nilijiuliza, “Hivi mimi ni mke au mpangaji tu wa nyumba hii?” Ndoa yangu ilikuwa imegeuka uwanja wa maumivu ya kimya. Mume wangu, ambaye zamani alikua rafiki yangu wa karibu, ghafla alianza kurudi nyumbani usiku wa manane. Saa tano, saa sita, saa saba… Bila ujumbe, bila simu, bila hata maelezo. Nikimuuliza, alikua na majibu makali kama vile: “Kwani wewe ni saa ya polisi?”
Awali nilidhani ni kazi. Baadaye nikaanza kuhisi kuna mwanamke mwingine. Nilianza kumfuatilia kwa macho, nikaanza kuhisi vitu ambavyo sikutaka kuvihisi kama mke. Kulikuwa na harufu za manukato ambazo si zangu, majina yasiyo ya kawaida kwenye simu yake, na tabia ya kuoga kabla hata ya kuniambia “hi.” Nilianza kupoteza amani.
Kilichoniumiza zaidi ni kuwa, hata ndani ya nyumba hakuwa tena yule wa zamani. Hakuniangalia machoni, hakuniambia maneno mazuri, hakupenda hata chakula nilichopika. Nilihisi kama niko single katika ndoa.
Nilijaribu kusoma vitabu vya ndoa. Nilihudhuria semina za wake. Niliomba sana. Lakini kila nilipojaribu, yeye alionekana kuzidi kuwa mbali. Mpaka siku moja nilimshuhudia mwenyewe akimpeleka mfanyakazi wao kazini, usiku wa saa tano. Nilipomuuliza, alijibu kwa ukali: “Si kila kitu ni lazima ukijue!” Soma zaidi hapa.


Post a Comment