Mayele: Nikirudi Yanga mashabiki watanipokea tu - EDUSPORTSTZ

Latest

Mayele: Nikirudi Yanga mashabiki watanipokea tu

Fiston Mayele

Ni kesho kutwa mechi za lala salama Yanga vs Tz prison na Simba vs Jkt tanzania unaanzaje kukosa kuzitazama mechi hizi live kwenye simu yako bonyeza hapa kudownload app itakayo onesha mechi hizi zote live bureeee kabisa pia kwenye app hii kuna yale mambo yetu yale bofya sasa kuidownload mapema ili kuepuka usumbufu

Msikie mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Fiston Mayele raia wa Congo DR ambaye kwa sasa anasakata kabumbu la kulipwa Pyramids FC ya Misri.

"Pamoja na kwamba kumekuwa na vita kubwa juu yangu kwenye mitandao ya kijamii, bado naamini kwa asilimia 100% kwamba nikirudi Yanga mashabiki watanipokea.

"Kitu ambacho nimejifunza Tanzania ni kwamba mashabiki wengi huwa wanajali maslahi yao na sio ya wachezaji.

"Kucheza misimu miwili ndani ya yanga ilikuwa ni furaha sana kwao, ila ilipofika hatua ya mimi kuondoka, watu walianza kunichukia bila sababu yoyote.

"Mbona wachezaji wengi tuu wanaenda pale na kuondoka ila mimi tuu ndo wawe na chuki kubwa na mimi!!?, kosa langu kubwa liko wapi?


"Japo kuwa naamini kabisa nikirudi napokelewa kwa sababu narudisha maslahi kwenye upande wa timu na mashabiki, ila sidhani kama wanachokifanya ni sahihi," amesema Mshambuliaji wa zamani wa @yangasc Fiston Mayele.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz