Ahmed: Tutaanza kutoa 'Thank You' wiki ijayo - EDUSPORTSTZ

Latest

Ahmed: Tutaanza kutoa 'Thank You' wiki ijayo

Ahmed: Tutaanza kutoa 'Thank You' wiki ijayo

Ni kivumbi na Jasho jumapili hii ni Yanga vs Azam Fc mechi ya kibabe mechi ya kisasi ni fainali itakayo sisimua kila upande usikose kuitazama mechi hii live bureee kabisa kupitia simu yako bonyeza hapa kujiunga na group letu la telegram ili uweze kutumiwa app yenye chanel zote za azam tv na dstv buree ili uweze kuangalia mechi hii live bure kwenye simu yako pia yale mambo yetu yale yapo

Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amebainisha kuwa kuanzia wiki ijayo wataanza kutangaza majina ya wachezaji, viongozi, na benchi la ufundi ambao wataondoka na watakaoingia kuimarisha timu hiyo.

Ahmed amesema hayo jana baada ya Ligi Kuu kutamatika huku Simba wakimaliza nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo ambapo wameangukia kwenye michuano ya kombe la shirikisho Afrika ambayo watashiriki msimu ujao jambo ambalo amesema hayakuwa malengo yao kabisa.

“Kila kitu muda wake ukifika tutaweka hadharani, kwa sasa tunamshukuru Kocha Mgunda na Selemani Matola na benchi zima la ufundi, wamefanya kazi kubwa sana kuifanya Simba kumaliza katika nafasi hiyo. Wachezaji wote wa Simba wamepambana lakini haikuwa riziki na kumaliza nafasi hiyo ya tatu.

“Taarifa rasmi, mipango yote ya Simba tutaanza kuiweka rasmi baada ya ligi kumalizika. Tuiache wiki hii ipite lakini kuanzia wiki ijayo tutaanza rasmi kuachia taarifa rasmi nani tunamuondoa.


“Simba tumemaliza ligi vibaya, mtasikia taarifa nyingi sana huyu anaondoka huyu anakuja lakini tutulie. Maamuzi ambayo tutayafanya yatakuwa sahihi kwa maslahi ya Simba,” amesema Ahmed.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz