Droo ya Robo Fainali CAFCL kufanyika Machi - EDUSPORTSTZ

Latest

Droo ya Robo Fainali CAFCL kufanyika Machi

 Droo ya Robo Fainali CAFCL kufanyika Machi

Download app yetu Kutazama mechi ya Simba vs Galaxy na Al ahly vs Yanga live bure kwenye app yetu bofya hapa Sasa kuidownload

Klabu ya Soka ya Young African imeweza kushida mechi muhimu dhidi ya CR Belouizdad na kuweza kufikisha alama 8 kukaa nafasi ya pili katika kundi lake.

Kwa matokeo haya Yanga umeunga na Al Alhy kuingia moja kwa moja robo fainali ya CAF Champions League kabla ya mechi baina yao hao hao Weekend ijayo Jijini Cairo nchini Egypt.

Kikanuni Yanga haihitaji tena kitu chochote katika mchezo wa mwisho dhidi ya Al Alhy zaidi ya kama watashinda wanakuwa washindi wa kwanza wa kundi basi ambapo itawasaidia kucheza na mshindi wa pili wa kundi jingine na kuanzia ugenini kisha kumalizia nyumbani.

KANUNI ZINAWABEBAJE YANGA

Mchezo wa kwanza, CR Belouizdad 3 - 0 Yanga na mchezo wa pili Yanga 4 - 0 Belouizdad.

Hii ina maana katika head 2 head kuwa Yanga amemazidi Belouizdad kwa holi moja hivyo hata CR Belouizdad washinde mchezo wa mwisho wanafikisha point 8 ambazo Yanga tayari anazo ila hata afunge magoli mangapi hawezi kuwa juu ya Yanga hivyo ndio utaratibu unavyombeba Yanga kwenda Robo Fainali.

UTARATIBU WA DROO

Kabla ya kuanza kwa hatua ya mtoano (robo fainali) itakayoanza machi 29, 2024, droo ya kupanga michezo ya robo fainali itachezeshwa mmapema mwezi Machi katikati ili kujua kila timu inacheza na nani kwa kufuata yafuatayo:


✅Timu za kundi moja haziwezi kukutana

✅Timu zote mshindi wa pili kwenye Kundi zitaanzia nyumbani

✅Kila timu itapangiwa mpinzani mmoja kati ya Watatu waliopo

Timu zilizofuzu mpaka sasa;

✅Petro Luanda - Angola

✅ ASEC Mimosas - Ivory Coast


✅ TP Mazembe - Congo DR

✅ Al Ahly - Misri

✅ ⁠Mamelodi Sundowns - Afrika Kusini

✅ ⁠Yanga SC - Tanzania.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz