Taarifa Mpya kutoka Yanga ni kuhusu Okrah - EDUSPORTSTZ

Latest

Taarifa Mpya kutoka Yanga ni kuhusu Okrah

  

Nyota mpya wa Yanga Augustine Okrah ameanza mazoezi na kikosi cha Yanga kilichorejea mazoezini mwanzoni mwa wiki hii baada ya mapumziko ya takribani wiki mbili

Okrah yuko timamu kiafya baada ya kupona majeraha aliyopata katika michuano ya kombe la Mapinduzi


Kiungo huyo mshambuliaji aliyetua Yanga akitokea klabu ya Bechem United ya Ghana, anafanya mazoezi kwa ari kubwa


Okrah anafahamu haitakuwa rahisi kwake kujihakikishia nafasi ya kucheza kwenye kikosi cha kwanza kama hatajituma mazoezini


Ujio wake umemuongezea machaguo ya mawinga Kocha Miguel Gamondi ambaye ndiye alieidhinisha usajili wa nyota huyo wa zamani wa Simba


Okrah pia anaweza kutumika kama namba 10, nafasi ambayo Gamondi humtumia zaidi Aziz Ki na wakati mwingine Pacome Zouzoua



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz