Alichokisema Kocha mkuu wa Yanga baada ya kupoteza mechi dhidi ya IHEFU Fc - EDUSPORTSTZ

Latest

Alichokisema Kocha mkuu wa Yanga baada ya kupoteza mechi dhidi ya IHEFU Fc

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema wamepoteza mchezo dhidi ya Ihefu Fc kwa kuwa walifanya makosa ndani ya uwanja na sio kwa sababu alifanya 'rotation' ya kikosi chake


Katika mchezo huo uliopigwa uwanja wa Highland Estates, Mbarali Mbeya, Gamondi alibadili takribani wachezaji saba walioanza katika mchezo uliopita kwenye ligi ya mabingwa dhidi ya Al Merrikh


"Tumepoteza mchezo sio kwa sababu nimefanya mabadiliko ya kikosi, tumefungwa kwa sababu tulifanya makosa"


"Nafikiri bao la kwanza tuliwapa zawadi, tulizungumza mapema kuwa uwanja haukuwa rafiki kwetu hivyo tuepuke kucheza kwenye eneo letu lakini yakafanyika makosa ambayo yalipelekea tukafungwa"


"Bao la pili lilikuwa shambulizi la kushitukiza, hatukufanya vile ambavyo tulipaswa kufanya na kupelekea tukaadhibiwa"


"Kama tungepata ushindi leo hakuna mtu angezungumzia mabadiliko. Wakati mwingine ni muhimu kufanya mabadiliko haya kwa kuzingatia ratiba inayotukabili," alisema Gamondi


Gamondi aliongeza kuwa haukuwa mchezo wa kuvutia hasa kwenye kipindi cha pili pale Ihefu Fc walipoamua mpira usichezwe na waamuzi kuacha kuchukua hatua


"Sisi tumepoteza mechi uwanjani lakini kulikuwa na matukio mengine sana yasiyo ya kimichezo inasikitisha kuona hakuna hatua zilizochukuliwa," alisema



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz