Taarifa Mpya kuhusu Majeraha ya Skudu makudubela - EDUSPORTSTZ

Latest

Taarifa Mpya kuhusu Majeraha ya Skudu makudubela

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Jana kiungo wa Azam Fc James Akaminko aliwanyima Wananchi wa Tanga kushuhudia burudani kutoka kwa Waziri wa raha Skudu Makudubela ambaye aliumia kwenye dakika ya tano ya mchezo wa nusu fainali ya Ngao ya Jamii akifanyiwa madhambi na Akaminko


Skudu alishindwa kuendelea na mchezo huo kulazimika kutolewa nje kwenye dakika ya saba nafasi yake ikichukuliwa na Chrispine Ngushi


Uongozi wa Yanga umebainisha kuwa Skudu anaendelea vizuri ambapo atafanyiwa vipimo zaidi leo


Daktari wa Yanga Moses Etutu amesema Skudu alipewa dawa ya kutuliza maumivu ya goti, hali yake ikiwa ni nzuri sasa


Hata hivyo Etutu amesema watamfanyiwa vipimo zaidi baada ya saa 24 ili kubaini kama atahitaji matibabu zaidi au apewe mapumziko tu


Skudu huenda akarejea tena uwanjani kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Simba au Singida FG siku ya Jumapili



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz