Msemaji wa Yanga awatupia Dingo Azam Fc baada ya kuondolewa kwenye mashindano ya CAF - EDUSPORTSTZ

Latest

Msemaji wa Yanga awatupia Dingo Azam Fc baada ya kuondolewa kwenye mashindano ya CAF

Ally Kamwe.

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Ofisa Habari wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe amewatupia dongo Klabu ya Azam baada ya kuondolewa kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na Klabu ya Bahri ya nchini Ethiopia jana usiku kwa mikwaju ya penati.


Kamwe amedai kuwa kwa vile Uwanja wa Azam Complex unatumiwa na Yanga, basi ubadilishwe jina na kuitwa Yanga Complex Chamazi mpaka pale ambapo Yanga italerejea kutumia dimba la Mkapa ambalo linakarabitwa.


"Tunatuma maombi kwa TFF na Bodi ya Ligi ule uwanja ubadilishwe kuanzia sasa uitwe Yanga Complex. Tunakwenda kimataifa, tukiulizwa na CAF, Yanga ni timu, je, hii Azam ni nini? Tutajibu nini? Ni kiwanda au nini? Kwa hiyo tutaita Yanga Complex mpaka tutakapoondoka pale.


"Azam hakuna timu pale, kesho (leo) tukutane Yanga Complex Chamazi, anayebisha alete timu pale. Kesho (leo) tunakwenda kutambulisha Maxi Day pale na kuutambulisha rasmi ule kuwa uwanja wetu," amesema Kamwe.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz