Matokeo ya Simba vs Power Dynamos Leo August 06 - EDUSPORTSTZ

Latest

Matokeo ya Simba vs Power Dynamos Leo August 06

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Simba imehitimisha Tamasha la Simba Day kwa ushindi mnono wa mabao 2-0 dhidi ya Power Dynamos katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Ilikuwa siku maalum kwa mashabiki wa Simba kuishuhudia timu yao kwa mara ya kwanza baada ya maboresho

Kwa hakika dalili njema zimeonekana mapema, huu unaweza kuwa msimu bora kwa Wanamsimbazi

Willy Onana alihitaji dakika tano tu kuifungia Simba bao la kuongoza akipiga shuti lililomshinda mlinda lango kutoka nje kidogo ya 18

Simba ilitwala mchezo huo nyota wapya Onana na beki Che Malone Fondoh wakiwa kivutio kwenye kipindi cha kwanza


Bao la pili lilifungwa na yuleee namba sita, ambaye watu walipokwa uwanja wa ndege, Fabrice Ngoma

Ngoma alifanya uamuzi sahihi wa kutua Simba badala ya kule upande wa pili kwani jambo la uhakika ni kuwa msimu huu yuko kwenye kikosi bora na atashiriki mashindano makubwa 'Super League'


Ulikuwa mchezo ambao pengine Simba ingeweza kuondoka na ushindi mnono zaidi kwa idadi ya nafasi walizotengeneza

Luis Miquissone 'Konde Boy' kwa mara nyingine leo Wanasimba wamemuona baada ya kurejea

Alifanya majaribio kadhaa kwenye lango la Power Dynamos lakini haikuwa bahati kwake kuzifumania nyavu

Ilikuwa siku iliyojaa burudani kwa Wanasimba kuanzia asubuhi na kuhitimishwa kwa ushindi


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz