Hatujakurupuka kuzindua jezi mlima Kilimanjaro - Ahmed - EDUSPORTSTZ

Latest

Hatujakurupuka kuzindua jezi mlima Kilimanjaro - Ahmed

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema uamuzi wa kwenda kuzindua jezi juu ya kilele cha Mlima Kilimanjar umezingatia maslahmi mapana ya nchi


Ahmed amesema katika misimu sita iliyopita, Simba imetangaza Utalii Tanzania kupitai Visit Tanzania, huu ni wajibu kwa klabu kutangaza utalii wa Tanzania


Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Ahmed ameandika ujumbe huu;


"Wengi wanadhani tumeamua kuzindua jezi Juu ya Mlima Kilimanjaro kwa lengo la kujibu mapigo ya wale waliogawa jezi Lilongwe"


"Kwa miaka sita sasa tumekua tukibeba bendera ya utalii wa nchi kupitia Visit Tanzania. Sisi tunaamini tunaowajibu wa kuisaidia Serikali yetu kutangaza Utalii wetu"


"Tangu tumetangaza kuzindua jezi juu ya Mlima Kilimanjaro, taarifa imesambaa dunia nzima na kila mmoja anahamu ya kushuhudia tukio hilo Kuzindua Jezi juu ya Mlima"


"Ni tukio la kwanza duniani, hivyo dunia nzima inasubiri kushuhudia itakuaje Wakati wanashuhudia uzinduzi wa jezi, hapo hapo wanaushuhidia uzuri wa Mlima Kilimanjaro"


"Tukio litakua Mubashara kupitia channel zote za Simba hivyo watu watakiona kilele cha Mlima Kilimanjaro. Tunaamini kwa tukio hili wengi watavutiwa na kuhamasika kupanda Mlima Kilimanjaro Na hapo Simba tutakua tumetimiza malengo yetu," aliandika Ahmed



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz