Ahadi ya kocha mkuu wa Yanga baada ya kutambulisha Rasmi Jangwani - EDUSPORTSTZ

Latest

Ahadi ya kocha mkuu wa Yanga baada ya kutambulisha Rasmi Jangwani

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema ana furaha kujiunga na mabingwa hao wa Tanzania Bara kwa misimu miwili mfululizo na yuko tayari kuanza majukumu yake


Gamondi amesema ameifuatilia Yanga iliposhiriki michuano ya CAF msimu uliopita na alifurahishwa na maendeleo na zaidi mipango ya timu


"Nafurahi kujiunga na Yanga, nimeifuatilia Yanga na najua malengo makuu msimu huu ni kufanya vizuri kwenye Ligi ya Mabingwa. Pia nimefurahishwa na mikakati ya timu wakati nilipozungumza na Rais"


"Naamini baada ya kupata mapumziko kutokana na kufanya kazi mfululizo katika nchi mbalimbali, huu ni wakati sahihi kupata changamoto mpya"


"Nipo hapa kufundisha kandanda safi, kuwapa furaha mashabiki na kushinda makombe, naamini tunaweza kufanikiwa malengo yetu," alisema Gamondi


Baada ya Gamondi kutua, wakati wowote Yanga itatangaza benchi lake la ufundi tayari kuanza maandalizi ya msimu mpya (2023/24) ambapo wachezaji wanatarajiwa kuingia kambini Avic Town siku ya Jumatatu



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz